Afisa Mtendaji wa mtaa wa Mbezi Msumi ashambuliwa hadi kufa ofisini kwake

MAUAJI ya kutisha yametokea eneo la Mbezi Msumi mkoani Dar es Salaam baada ya watu wasiofahamika kudaiwa kuvamia ofisi za Serikali ya Mtaa wa eneo hilo na kisha kumuua Ofisa Mtendaji kwa kumkata na panga.

Tukio hilo la mauaji limetokea leo Oktoba 11, 2021 kati ya saa sita hadi saa saba mchana wa leo na inadaiwa ofisa huyo mtendaji wa Serikali ya Mtaa wa Mbezi Msumi ameshambuliwa kwa kukatwa na panga shingoni na watu ambao hawahamiki.

Akizungumza na Michuzi TV pamoja na Michuzi Blog leo Mmoja wa mashuhuda na mwananchi wa eneo hilo(jina limehifadhiwa) amedai wameshangazwa na tukio hilo la mauaji ambalo limefanywa kwa kiongozi huyo.

Alipoulizwa iwapo watu waliofanya tukio wamefahamika, amejibu hawajafahamika kwani baada ya kutekeleza unyama huo walikimbia na haijulikani ni akina nani na wametoka wapi, ingawa anaamini Jeshi la Polisi linajua namna ya kufuatilia tukio hilo na kuupata ukweli.

"Wananchi tumejawa na taharuki baada ya kutokea tukio hili la mauaji , hatuji nini kimesababisha hadi watu hao kufanya unyama huu kwa kiongozi wa Serikali ya Mtaa,tupo hapa tunasubiri kuona nini kinachoendelea,"amesema shuhuda huyo alipokuwa akizungumza na Michuzi TV

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni Ramadhan Kingai aliyezungumza na Michuzi TV amethibitisha kupata taarifa hizo za tukio la mauaji na tayari askari polisi tayari wako eneo la tukio."Tumepata taarifa za tukio hilo,tunafuatilia na baadae tutatoa taaria rasmi kwa vyombo vya habari."

Michuzi TV na Michuzi Blog inaendelea kufuatilia tukio hilo kwa karibu ili kuhakikisha umma wa Watanzania unafahamu ukweli wa tukio hilo kupitia Jeshi la Polisi ambalo limeanza kufuatilia.
Lol
 
Wa Tz huwa wanapenda kujidai wajuaji sana wazee wa kutoa hukumu utaskia huyo kadhulumu kiwanja au katembea na mke wa mtu, ukiuliza alidhulum nn?

Hawan majibu zaid ya kuhisi kama muuaji alikua muuza mazao hapohapo watasema alidhulum mazao
Yan akilin kwao huwa hawajui hata mtenda haki anamaadui au pia anae dhulumiwa anaweza kuuwawa
Hata Hamza alipouwawa na polisi wananchi siku ile ile walichunguza na kusema alidhulumiwa madini, na wakalaumu polisi kwanini walimuua.
Ila yeye kuua askari 4 ilikuwa haina shida.

Nyerere hakutuachia utamaduni wa aina hii hata sijui tumeutoa wapi.Hivi sasa watumishi wa serikali yanapowafika mabaya watanzania tumekuwa watu wa kushangilia na kuwatetea wahalifu kuwa walichofanya ni sahihi.

Huyo mtendaji Kama angeweza kujihami na kufanikiwa kuwaua hao wahalifu leo tungesikia analaumiwa kwa kuchukua sheria mkononi, mara hawakumvamia amewaua kuficha ukweli juu ya dhuluma aliyowafanyia.

Hivi karibu Kuna tukio lilitokea la askari magereza wawili kutuhumiwa kubaka, hata hivyo ile ilikuwa ni tuhuma tu inaweza kuwa kulikuwa na makubaliano ambayo hayakufikiwa hivyo binti akaamua kusema alibakwa. Lakini wanachi walichunguza na kuhukumu siku hiyo hiyo ila tukio hilo angekuwa mlalamikaji ni askari watu wangekuwa upande wa mtuhumiwa.

Tuache chuki dhidi ya serikali na watumishi wa umma, haya mambo yanaanza kidogo kidogo tunaendelea kurithisha vizazi vyetu itafika hatua hatutaweza kuyarekebisha.

Tukumbuke uhalifu hauna macho.
 
Hata Hamza alipouwawa na polisi wananchi siku ile ile walichunguza na kusema alidhulumiwa madini, na wakalaumu polisi kwanini walimuua.
Ila yeye kuua askari 4 ilikuwa haina shida.

Nyerere hakutuachia utamaduni wa aina hii hata sijui tumeutoa wapi.Hivi sasa watumishi wa serikali yanapowafika mabaya watanzania tumekuwa watu wa kushangilia na kuwatetea wahalifu kuwa walichofanya ni sahihi.

Huyo mtendaji Kama angeweza kujihami na kufanikiwa kuwaua hao wahalifu leo tungesikia analaumiwa kwa kuchukua sheria mkononi, mara hawakumvamia amewaua kuficha ukweli juu ya dhuluma aliyowafanyia.

Hivi karibu Kuna tukio lilitokea la askari magereza wawili kutuhumiwa kubaka, hata hivyo ile ilikuwa ni tuhuma tu inaweza kuwa kulikuwa na makubaliano ambayo hayakufikiwa hivyo binti akaamua kusema alibakwa. Lakini wanachi walichunguza na kuhukumu siku hiyo hiyo ila tukio hilo angekuwa mlalamikaji ni askari watu wangekuwa upande wa mtuhumiwa.

Tuache chuki dhidi ya serikali na watumishi wa umma, haya mambo yanaanza kidogo kidogo tunaendelea kurithisha vizazi vyetu itafika hatua hatutaweza kuyarekebisha.

Tukumbuke uhalifu hauna macho.
Binadam ndo tulivyo huwa hatuishiwi Cha kusema ila kuvithibitisha tunavyo visema ndo huwa ni ngumu maana vingi n vya uongo na havna uthibitisho na hat ukweli ukidhihirishwa bado watu wataukataa na kuendelea kuamini hisia zao
 
Back
Top Bottom