Dalton elijah
JF-Expert Member
- Jul 19, 2022
- 780
- 1,831
Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga imefanikiwa kumfanyia upasuaji na kumtoa mwanamke mwenye miaka 55 ujauzito aliodumu nao kwa miaka minne.
Kwa mujibu wa Daktari Bingwa wa Magonjwa ya akina Mama na Uzazi wa hospitali Augustino Maufi amesema ujauzito huo uliokuwa na uzito wa kilogramu 1.6 ulitunga nje ya mfuko wa uzazi na baada ya kufanyika kwa upasuaji huo kiumbe kilichokuwa ndani ya ujauzito huo kilikutwa kimeshafariki.
Mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji huo ambaye jina lake limehifadhiwa amedai kuwa kabla ya kwenda hospitali kufanyiwa upasuaji alikuwa akienda kwa waganga wa tiba mbadala kwa ajili ya kumaliza tatizo la maumivu ya tumbo na kusita kwa hedhi kwa kipindi kirefu kabla ya mganga aliyekuwa anamtibia kufariki dunia na yeye kulazimika kugeukia hospitali.
Dkt. Maufi ametoa wito kwa watu wanaofanya tiba mbadala kuhakikisha wanawashauri wagonjwa wao kufika hospitalini kwa ajili ya matibabu zaidi pindi inapotokea wamekosa namna nzuri ya kuwasaidia lengo ikiwa ni kuokoa maisha yao.
Sources :Azam Tv
Kwa mujibu wa Daktari Bingwa wa Magonjwa ya akina Mama na Uzazi wa hospitali Augustino Maufi amesema ujauzito huo uliokuwa na uzito wa kilogramu 1.6 ulitunga nje ya mfuko wa uzazi na baada ya kufanyika kwa upasuaji huo kiumbe kilichokuwa ndani ya ujauzito huo kilikutwa kimeshafariki.
Mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji huo ambaye jina lake limehifadhiwa amedai kuwa kabla ya kwenda hospitali kufanyiwa upasuaji alikuwa akienda kwa waganga wa tiba mbadala kwa ajili ya kumaliza tatizo la maumivu ya tumbo na kusita kwa hedhi kwa kipindi kirefu kabla ya mganga aliyekuwa anamtibia kufariki dunia na yeye kulazimika kugeukia hospitali.
Dkt. Maufi ametoa wito kwa watu wanaofanya tiba mbadala kuhakikisha wanawashauri wagonjwa wao kufika hospitalini kwa ajili ya matibabu zaidi pindi inapotokea wamekosa namna nzuri ya kuwasaidia lengo ikiwa ni kuokoa maisha yao.
Sources :Azam Tv