happiness win
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 2,461
- 1,394
Nilikuwa na msichana wa kazi niliyeishi naye kwa miaka 5. Kwa bahati mbaya hana wazazi wala ndugu anayeweza kumsaidia au kumtegemea kwa lolote. Mwaka jana alipata mimba na nilipomhoji kijana aliyempa mimba alikubali na kuamua kumchukuwa na kuishi naye kwa tabu kwani Bwana hana kazi, ni mtu wa day waka tu.
Jana msichana ananipigia simu na kunieleza kuwa Bwana wake amejiunga na Kikundi cha Uamsho na ametoa amri inayomtaka Mdada kubadili dini (alikuwa Mksristo) mara moja la sivyo aondoke na mtoto wake wa miezi miwili. Mdada hana pa kwenda na hayuko tayari kubadili dini. Nishaurini nimwambie afanye nini?
Jana msichana ananipigia simu na kunieleza kuwa Bwana wake amejiunga na Kikundi cha Uamsho na ametoa amri inayomtaka Mdada kubadili dini (alikuwa Mksristo) mara moja la sivyo aondoke na mtoto wake wa miezi miwili. Mdada hana pa kwenda na hayuko tayari kubadili dini. Nishaurini nimwambie afanye nini?