Ukifuatilia mapokeo ya hii dhana ya NRNE, unagundua nchi yetu ina changamoto kubwa ya uelewa wa mambo. Inawezekana pamoja na sababu kadhaa kiwango chetu cha uelewa wa mambo na kufanya maamuzi sahihi ni miongoni mwa sababu zinazotufanya tuendelee kuwa maskini.
Hawa wapuuzi CHADEMA wametuletea hii dhana yao ya NRNE ambayo kwa mtizamo wangu ni dhana ya kuamsha tafakari miongoni mwa watanzania juu ya mifumo yetu ya uchaguzi. Hii ni kuhusu je, hapa nchini tuna 'UCHAGUZI', je, unakidhi vigezo vyote vya kuitwa uchaguzi?, je, wadau wote kwa maana ya mpiga na mpigiwa kura, wasimamizi na waangalizi wanaridhika na mchakato mzima wa chaguzi zetu?. Sasa hawa wajinga wa CDM wao ktk maswali hayo yote wamejipa jibu la No, ndipo wanakuja na hitimisho la nini kifanyike ili ionekane kweli kuna uchaguzi na ilo hitimisho lao ndio hii dhana ya NRNE.
Sasa kinachofanywa na baba yangu kamanda hapo, waandishi wa habari, sisi tunaojadili hapa na viongozi wetu kuendelea kujadili ili suala kimantiki yake au vinginevyo ni kuendelea kuwapa ushindi hawa manyumbu wa ufipa. Nionavyo, ktk movement nyingi walizokuja nazo hawa wapuuzi, hii ndio yenye mafanikio makubwa sana. Kivipi, mjadala na tafakuri ya NRNE haitoisha leo wala kesho, na itapamba moto zaidi mara tu baada ya uchaguzi wa Octoba kukamilika.