Nimesikia Clouds FM Afande Kova amekataa kutoa the so called Kibali cha maandamano ya kesho saa mbili asubuhi na kusema kuwa hakuna kiongozi wa juu wa Serikali aliyeyakataa madai ya katiba mpya hivyo hakuna haja ya kuandamana.
Hivi?????
Huyu ndugu haya mamlaka kayatoa wapi?
Polisi huyu, kamanda huyu, haya mamlaka ya kutafsiri hisia za wananchi na kuyafanyia maamuzi kana kwamba yeye ndio mahakama kayatoa wapi????
Huu kama si ukuadi kwa serikali nini?
Ninavyoelewa na kwa kadiri katiba ya nchi inavyoelekeza, kinachoombwa kwa polisi si kibali bali ni wananchi kutoa taarifa ya dhamira yao kufanya maandamano (kueleza hisia) na polisi wanawajibika kutoa ulinzi na kuhakikisha amani inatamalaki katika hiyo shughuli ya kutekeleza uhuru wa kikatiba na si vinginevyo...
Majukumu ya polisi yanaishia hapo kulinda amani basi!!!
Huyu ndugu huu upupu kautoa wapi?
Nawasilisha
Hivi?????
Huyu ndugu haya mamlaka kayatoa wapi?
Polisi huyu, kamanda huyu, haya mamlaka ya kutafsiri hisia za wananchi na kuyafanyia maamuzi kana kwamba yeye ndio mahakama kayatoa wapi????
Huu kama si ukuadi kwa serikali nini?
Ninavyoelewa na kwa kadiri katiba ya nchi inavyoelekeza, kinachoombwa kwa polisi si kibali bali ni wananchi kutoa taarifa ya dhamira yao kufanya maandamano (kueleza hisia) na polisi wanawajibika kutoa ulinzi na kuhakikisha amani inatamalaki katika hiyo shughuli ya kutekeleza uhuru wa kikatiba na si vinginevyo...
Majukumu ya polisi yanaishia hapo kulinda amani basi!!!
Huyu ndugu huu upupu kautoa wapi?
Nawasilisha