Adhabu za wanajeshi

Humo ndani ya kambi nahisi kulikuwa na mzito yupo ndani, na muda wowote alitakiwa kutoka. Kama kungekutwa geti limezibwa vile angezinguliwa vibaya na hata kutukanwa. Kuliko aje kuzinguliwa lazima akuzingue wewe
 
Tena wewe ndiyo utakuja kuumizwa kabisa ukileta ujinga huo. Kule kuna watu wameshindikana na zaidibya wahuni, ukitaka ukae nao wale kwa amani punguza ujuaji
Hakuna kitu hapo, watz acheni uoga wa kijinga, ndo maana mnaonewaga kifala kisa ya uoga, mwanajeshi ni binadam kama binadam mwingine tuu, akijilengesha kwenye 18 unaweza kumua na akafa kama wanavokufa binadam wengine
 
Sasa hivi sifa ni pesa sio upot, aje na upot wake aje na mwenye pesa zake hata Dem, alaf tuwafungulie mbwa wakali tuone ni nani atakaeng'atwa

yani hapo lazma pot ang'atwe na upot Wake maana hana pesa.
Unachoshupalia ni nini hapa?kwani huyo dereva hakutenda kosa?ushaambiwa ukitenda kosa kwenye eneo lao ww unakazania huwaogopi cha kufanya kakojoe pale kambini kwao utuletee mrejesho
 
Hakuna kitu watz acheni uoga wa kijinga, ndo maana mnaonewaga kifala kisa ya uoga, mwanajeshi ni binadam kama binadam mwingine tuu, akijilengesha kwenye 18 unaweza kumua na akafa kama wanavokufa binadam wengine
Wewe upo hapo nyuma ya keyboard unajiona ni jasiri sana, sasa mimi nakwambia nishawahi kukaa nao jamaa kwenye mafunzo huko walikuja watu watata sana na watukutu kupitiliza ila baadaye walikuwa wapole. Hao jamaa waone hivyohivyo na magwanda yao kama mabishoo ila wameshindikana. Kama unataka amani na kutetea haki yako kuwa mpole na upeleke malalamiko baadaye kwa wakubwa zao atashughulikiwa hata kupoteza kazi. Sasa wewe jitie una ujasiri wa waandamanaji wa UKAWA, utakuja kusimulia
 
Hahaha umenikumbusha kuhusu JITE UTE.

Mie nimepiga pale 6 years yaan O and A levels.

Kuna kale kazee kanajiita NDYAMKAMA yule mzee alijaa ktk 18 zetu tulimla mitama sana nje ya ukuta. Kimbembe wiki iliyofuata. Tulikoma.


Hahah kuhusu canteen aisee nilikuw nakimbizana na wale Service na private flan hivi muda umeisha wa kula ila unakimbia na bakur la supu (SUPU ya kioo) huku na kule..


Smart Area pale.. aiseee uwanja wa DAMU palee kuna siku Kondakta alijichanganya wauni wakashuka nae wakamuingiza ndani mule. Kilichomtokea nahisi alibadiri ruti ya daladala kesho yake.
 
Ukiacha hilo la huyo Kapteni kukuonea hayo galiyobaki yote ni makosa na ilikuwa ni sahihi kabisa kutandikaa. Jitegemee kabla ya hujaanza kusoma na hata sare hamjapewa unasomewa sheria zote za shule, wewe inaonekana ulikwepa siku za mwanzo kuijua shule
 
Watu Kama wewe ndiyo mnakuwaga wapole Kama mmemwagiwa maji mkiwaona bakabaka. Ila kwa background mnaandika kishujaa Kama hivi.

Keyboard warrior.
 
 
Nakumbuka 2009 nikiwa ndani ya kigoma, nilipewa adhabu ya kujaza pipa kwa kijiko...


Ntaludi kumalizia but usiombe ujae angle za hao jamaa.
Dodoma makutupora iyo 2010 raia kapewa kisoda ajaze ndoo ya lita 20 maji umbali wa kama hatua 30 ivi kutoka bombani adi ndoo ilikowekwa.. Kwa kosa la kuzurura eneo la jeshi
 
We bado mshamba!! Siku hizi mwanajeshi Hana maajabu yoyote akijichanganya anapigwa tu
Uliza mtoni mtongani walivofunga mitaa kwa kosa la mwana jeshi kukabwa na kuuwawa relini... Usijidanganye kupiga mwana jeshi.. Labda uwe hukai mitaa hiyo
 
Zaman nikiwa na miaka 16 tulienda kutafuta magoli ya miti, kwakua kambi za jeshi huwa kuna mapori fulan tukaenda kukata huko.

Wakati tumemaliza kukata yale magoli tunarudi tukakutana na mjeshi mmoja amevaa sare zao ila sio hizi za kijeshi nahisi atakua na cheo yule jamaa.

Akatuuliza mnatoka wapi? Tukasema tumekuja kuchukua magoli tukacheze mpira,, pale tulipokutana nae kulikua na kibao kimeandikwa "eneo hili ni Mali ya JWTZ, ni marufuku kukata miti, kuchunga mifugo na kupita eneo hili kuanzia sa 12 jioni".

Yule mjeshi akaanza kutuliza maswali tukawa tunajibu fresh tu,akasema tusome kile kibao kwa sauti tukasoma mmoja mmoja kisha akaanza kuuliza swali mmoja mmoja, akaanza na mimi ulivokuja ulikiona hiki kibao? Nikajibu ndio nilikiona huku najitetea tusamehe, akasema kumbe ulikiona na ukakaidi haya ww kaa chini hapa .

Wale wenzangu walivoona nimeambiwa vile kwamba "'kumbe uliona kibao hiki na ukakaidi"walipoanza kuulizwa wao lile swali ulikona hiki kibao kila mtu akawa anajibu sikuona kibao kisha anaambiwa kaa upande huu, upande mwingine tofauti na mimi.

Yule mjeshi akasema kwakua ww umesema ulikiona hiki kibao nenda ila nyie wengine laleni chini huku anavunja yale magoli. Yale magoli ndo ilikua fimbo za kuwachapia, aisee walipigwa !! Nilikua nasikia tu sauti za mwangwi zinajirudia watu wanalia balaa. Unajua ukiwa porini ukiita kwa sauti huwa sauti kama inajirudia vile ndo ilivokuwa walipigwa vibaya sana na kuanzia siku hiyo mpaka nakuwa sikuwahi kukanyaga eneo lile.

Story ya pili nikiwa secondary, shule yetu ilikua barabarani sana, sasa siku hiyo saa 5 tumetoka kuna jamaa alikua anapita kavaa tshirt ya kijeshi akakutana pale shuleni na mwanajeshi akasimamishwa.

Yule jamaa kwanz akavuliwa ile tshirt alafu akambiwa aogelee kwenye yale madimbwi ya maji machafu barabarani yaani apige mbizi pale!! Jamaa akatii akaanza kugalagala pale kwenye maji machafu alafu asukutue yale maji akatii.

Baadae akaambiwa atangulie mbele waende jeshini akawa anamambiwa kimbia kisha anambiwa chuchumaa huku yule mjeshi anakuja mdogo mdogo sijui hata walifika wapi.

Ila kiukweli hatupaswi kufurahia huu upumbavu na uonevu, kwasasa siwezi kubali kuonewa kipuuzi hivo.

Kuna siku nipo soko fulan hapa dar mwanajeshi mmoja akaja na gari binafs akapaki gari vibaya mbele ya duka, yule jamaa wa dukan hakujua kama ni mwanajeshi maana alikua kavaa suruali ya jeshi na tshirt ya kawaida kwahyo alivokuwa ndani ya gari hauwezi jua kama ni mwanajeshi mpaka ashuke.

Yule jamaa wa dukan alimwambia tu vizuri oya usipaki hapo unaziba njia yule mwanajeshi akashuka kwa hasira kutoka kwenye gari. toka dukani jamaa akatoka dukan akamuomba msamaha baada ya kugundua ni mwanajeshi.

Sasa nikajiuliza mbona hamna kosa hapa la kuomba msamaha! na ukiangalia kweli kapaki vibaya pale.
 
Kaka usimalize maneno... Wako watu watata na wanajua mchezo ya hatari.. Ila ukiyaingia kwa wanajeshi Kua mpole
 
 
We bado mshamba!! Siku hizi mwanajeshi Hana maajabu yoyote akijichanganya anapigwa tu
Wajuaji Wenzio walipita eneo la jeshi pale Lugalo mida ya saa 12 jioni kigiza kimeshaanza kuingia,na Sheria ya like eneo halifuhusiwi watembea kwa miguu kukatiza mida mibovu(enzi hizo sijui siku hizi utaratibu upoje). Walikuwa wanapiga kigoma Cha Uruguay wakitokea kawe wanakatiza Lugalo wanaelekea kule juu makongo.

Walipofika mitaa ya Lugalo wakakutana na Askari wakaulizwa mnaenda wapi saa hizi,wakajibu makongo kwenye shughuli. Afande akawaambia sasa mnaonaje mngetuburudisha kidogo kabla hamjaondoka? Jamaa kwa sifa wakaona hakuna shida,kigoma kikapigwa.

Kigoma kikapigwa Hadi usiku,jamaa walipojisikia njaa wakapewa na msosi, wajomba wakawaambi endeleeni kutoa burudani. Wazee walipiga ngoma mpaka asubuhi hadi wakaanza kulia. Kesho take ndiyo waliachiwa wakiwa mikono imevimba kwa kupiga ngoma.

Ungekuwepo katika hili kundi ungezichapa?
 
Watu kama ww ndo waoga balaa ila mkiwa mna type sasa mbwembwe nyingi, miaka ya nyuma walifunga mtaa wetu wote kisa mabomba yaliibiwa jeshini unafikiri mtaa mzima ni wajinga kutii kutotoka?

aisee usiombe ww mbona yalipatikana mabomba siku hiyo hiyo.
 
Ilitokea wapi hii brother?
 
Jamaa wana adhabu kali
But kuna mkuu XXX aliteuliwaga kwenda ule mkoa wa Kigoma na back ground yake alikuwa na cheo kikubwa tu huko baka baka.

Sasa kuna sehemu ziwani huko watu walikuwa wanalima nyanya na walikuwa hawaruhusiwi basi mheshimiwa akaenda na vijana wake wakaenda kufyeka nyanya zote ziwani.

Wazee walokuwa wanalima zile nyanya walikuwa wanaomba ziachwe ili wavune hivyo hvyo japo hazijakomaa waliambulia virungu na kuondoka lakini walitoa kauli moja tu kuwa tunaenda kukuroga jamaa kutokana na kujiamini na ile morali ya baka baka akawa anajibu mbovu wazee wakaondoka zao.

Baada ya week jamaa alipata mimba kila siku mimba inazidi kuwa kubwa kufika miezi 3 ikabidi wampeleke hosptal,wakamkuta kweli ana ujauzito kutokana na unyeti wa jambo alihamishwa mkoa kimya kimya na issue ilizimwa kimya kimya jpo watu wa mkoa huo baadhi wanakumbuka hilo.

So hapo kwa upande wangu ni kila mmoja asimame kwenye upande wake raia asimamie sehemu yake kama raia,na askari asimame kama mlinda raia na mipaka yake kama kiapo chake kinavyomtaka,ila kuendelea kuwasifia humu kwa wanavyofanya kinyume na sheria muwakumbushe pia kuna upande wa pili kwani si kila raia utamfanyia hilo atakubali.

Wengine utamfanyia hilo ataenda kukufanyia ya kukufanyia ukapoteza hata maisha huku ukiiacha familia yako ikiteseka kwa pension yako ya milioni 10 utayoiacha kutokana na mshahara wako wa laki 4
 
Anajifanya chizi😀
 
Watu kama ww ndo waoga balaa ila mkiwa mna type sasa mbwembwe nyingi, miaka ya nyuma walifunga mtaa wetu wote kisa mabomba yaliibiwa jeshini unafikiri mtaa mzima ni wajinga kutii kutotoka?

aisee usiombe ww mbona yalipatikana mabomba siku hiyo hiyo.
A Wapi mi sionewagi kipumbavu eti kisa mwanajeshi kwenye haki mi ni mkali Zaid ya Simba lazma haki itendeke
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…