Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,916
- 30,259
ADAM SHAFI KATIMIZA MIAKA 80: KALAMU YA SHAFI KATIKA KUIELEZA ZANZIBAR
Nilikuwa nimeanza kukisoma kitabu ‘’Haini,’’ cha Shafi Adam Shafi na haikunichukua muda kutambua kuwa mikononi mwangu nina kitabu ambacho ni ‘’masterpiece,’’ yaani kitabu kilichosheheni ujuzi wa hali ya juu sana katika uandishi.
Hapo hapo ikanijia hamu ya kuzungumza na mwandishi.
Adam Shafi namfahamu kwa kumuona lakini sina mazoea na yeye na nikatambua na yeye akiniona atanitambua.
Nikampigia simu jamaa yake Mohamed Mshangama kumuomba simu ya Shafi Adam Shafi.
Nikampigia.
Baada ya salamu na kujitambulisha jina bila ya kuweka ‘’nicities,’’ nikamwambia, ‘’Sheikh Shafi hivi unadhani wewe utamdanganya nani?
Wewe unaandika kitabu cha historia ya kweli kisha unasema hii ni ‘’fiction,’’ hadithi ya kutunga.
Utawadanganya wengine mimi nishatambua kuwa hiki kitabu ‘’Haini,’’ni mambo ya kweli kabisa.’’
Ikiwa wewe si Mswahili na huna mazoea na huyo mtu aliyekupigia simu na lugha yake ni kama hii kali ya ‘’wewe,’’ utapata shida ya kutambua ujumbe ndani ya maneno yale na huenda ukaghadhibika kuona mtu humjui anakupigia simu ya kukushambulia.
Nilikuwa nimeanza kukisoma kitabu ‘’Haini,’’ cha Shafi Adam Shafi na haikunichukua muda kutambua kuwa mikononi mwangu nina kitabu ambacho ni ‘’masterpiece,’’ yaani kitabu kilichosheheni ujuzi wa hali ya juu sana katika uandishi.
Hapo hapo ikanijia hamu ya kuzungumza na mwandishi.
Adam Shafi namfahamu kwa kumuona lakini sina mazoea na yeye na nikatambua na yeye akiniona atanitambua.
Nikampigia simu jamaa yake Mohamed Mshangama kumuomba simu ya Shafi Adam Shafi.
Nikampigia.
Baada ya salamu na kujitambulisha jina bila ya kuweka ‘’nicities,’’ nikamwambia, ‘’Sheikh Shafi hivi unadhani wewe utamdanganya nani?
Wewe unaandika kitabu cha historia ya kweli kisha unasema hii ni ‘’fiction,’’ hadithi ya kutunga.
Utawadanganya wengine mimi nishatambua kuwa hiki kitabu ‘’Haini,’’ni mambo ya kweli kabisa.’’
Ikiwa wewe si Mswahili na huna mazoea na huyo mtu aliyekupigia simu na lugha yake ni kama hii kali ya ‘’wewe,’’ utapata shida ya kutambua ujumbe ndani ya maneno yale na huenda ukaghadhibika kuona mtu humjui anakupigia simu ya kukushambulia.