GE2025 ADA TADEA tunagombea Urais Ili Kupata Nafasi ya Pili

GE2025 ADA TADEA tunagombea Urais Ili Kupata Nafasi ya Pili

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Dalton elijah

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
780
Reaction score
1,831
Mgombea urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ADA-TADEA, Juma Ali Khatib, amesema chama chake hakina dhamira ya kumpinga Rais wa sasa, Dk. Hussein Ali Mwinyi, bali kinalenga kupata nafasi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa fomu za kugombea urais katika Ofisi ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kwa Mwenyekiti wa Tume, Jaji George Kazi, Khatib alisema chama chake kimeamua kuwania urais ili kutimiza matakwa ya kisheria yanayowezesha mgombea kupata nafasi ya Makamu wa Kwanza wa Rais.

“Sisi katika chama ADA- TADEA tumeamua kugombea urais wa Zanzibar kwa lengo la ,kupata nafasi ya pili, kuwa makamu wa kwanza wa rais" amesema Khatib, akisisitiza kwamba ADA-TADEA haina sababu ya kumpinga Rais Dk. Mwinyi.

Chanzo: BBC
 
Mgombea urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ADA-TADEA, Juma Ali Khatib, amesema chama chake hakina dhamira ya kumpinga Rais wa sasa, Dk. Hussein Ali Mwinyi, bali kinalenga kupata nafasi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa fomu za kugombea urais katika Ofisi ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kwa Mwenyekiti wa Tume, Jaji George Kazi, Khatib alisema chama chake kimeamua kuwania urais ili kutimiza matakwa ya kisheria yanayowezesha mgombea kupata nafasi ya Makamu wa Kwanza wa Rais.

“Sisi katika chama ADA- TADEA tumeamua kugombea urais wa Zanzibar kwa lengo la ,kupata nafasi ya pili, kuwa makamu wa kwanza wa rais" amesema Khatib, akisisitiza kwamba ADA-TADEA haina sababu ya kumpinga Rais Dk. Mwinyi.

Chanzo: BBC
ahahahaa itakuwa CHAN
 
Aiseeeeh! Nchi ina vituko hii🙆‍♂️🙆‍♂️
 
Back
Top Bottom