Ada ndefu za shule balaa sijapata kuona

Musundi

JF-Expert Member
Dec 21, 2016
1,583
2,600
Nisamehewe bure kama nitaonekana nasukumwa na umaskini wangu kuandika haya ninayoandika.

Kiukweli nimeshangaa na kukwazwa kusikia kuwa kuna shule hapa hapa bongo inayotoza Tshs. 34 milioni kama ada ya mtoto wa chekechea tu na Tshs. 70 milioni ada ya mtoto wa sekondari.

Mwenzenu najiuliza maswali kadhaa:
1. Hivi ni wabongo wenzetu wa humu humu wanaosomesha katika shule hii?
2. Hivi mtoto anayesomeshwa hapa anapewa elimu kwa Mtaala tofauti na huu wa Wizara ya Elimu ya Tanzania?
3. Hivi mtoto anayesomea hapo anaandaaliwa kuja kuishi maisha hapa hapa bongo au mahali pengine ulimwenguni?
4. Hivi ni nini hasa cha ziada kinachohalalisha ukubwa wa ada kiasi chote hiki?
5. Hivi serikali yetu inayofahamika kutetea wanyonge imeridhia na kubariki utozaji wa ada wa kiasi hiki?

Kama kuna mwenye kunisaidia majibu ya maswali yangu, natanguliza shukurani kwa msaada.

I'm really puzzled, mwenzenu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
MKUU ACHA PESA IONGEE. WENGI WA WATOTO WANAOSOMA HAPO WANAANDALIWA KUWA MA CEOs WA BAADAE
 
Mil. 34 chekechea na mil. 70 secondary. Njoo na jina la hiyo shule vinginevyo hayo majungu
 
Kwa international school wanakosoma watoto wa mabarozi sawa. Lakini tuna shule nzuri local za binafsi Ada inabebeka. Usiofu!
 
We ni kubwa jinga!!

Hata akikutajia,hela tu ya kwenda school picnic au tours hutoweza kuchangia hata robo yake!!

Shwain!
Were unajua mil. 34 kwa chekechea ni hela ndogo? Hicho ni kiinua mgongo cha mtumishi. Hiyo ni hela ya kununua nyumba. Acha matusi ndugu mtanzania kwa mtu usiyemjua!
 
Hizo ni shule binafsi na international schools, zipo private schools zikiwa na ada afueni na zipo za serikali ambazo elimi bure.

Sasa unaiuliza serikali ili iweje? Kwani serikali ndio iliojenga shule? Inayolipa walimu wa hio shule? Au ndio inahudumia huduma za io shule?

Kwani umelazimika mtoto wako asome pale?
 
Back
Top Bottom