Ada elekezi shule binafsi tayari

Ada elekezi shule binafsi tayari

Hakuna cha ada elekezi wala Ada dekezi.Ukishindwa kumudu mpeleke government.Mnataka vitu vikubwa kwa bei chee?Kama unaona huduma haziendani na pesa unayotoa si umhamishie unakoona kunafaa?
 
Hamna kitu hapo, kwanini iwe majaribio na kwanini iwe kwa baadhi ya shule?

.....nilichokiona kuna shule zina sauti kuliko serikali....

Uko sahihi. Huu ni mwendelezo wa sanaa za maigizo za serikali ya Magufuli. Vigogo wengi katika 'chama' na serikali wanamiliki shule binafsi. Kwa lugha nyingine, hao hao wanaotuhadaa kuwa wana nia ya kudhibiti ada katika shule binafsi wana maslahi yao binafsi katika hizo shule! Hapa kuna mgongano wa kimaslahi na mwisho wa siku hakuna kitakachofanyika. Chini ya 'katiba ya Warioba' hii conflict of interest ingedhibitiwa kikatiba. Swali: kwanini CCM walikataa miiko na maadili ya viongozi katika rasimu ya Warioba?
 
Kwa mtazamo wangu sidhani kama hili swala la karo elekezi linawezekana......kwani tution fee itakuwa ndogo.....ila ukiangalia gharama za maradhi na chakula sidhani kama hapo kunaweza kuwa na mjadala!!!!
Katika shule zilizo bora....mtoto anakula milo minne!! Anapata matunda,maziwa nk.....
Maradhi mtoto analala chumba kimoja watoto wawili.....bafu zuri na choo cha maji safi.......kwa mazingira kama haya ni bora kumuambia mwenye shule afunge shule afanye biashara nyingine........kinyume na hapo naamini haitawezekana.

Mkuu ni maradhi au malazi..??
 
Serikali iachane na suala LA ada elekezi ya SHULE binafsi cha msingi iimarishe SHULE zake ziwe na kiwango safi madawati,mabweni,chakula kizuri,maabara,maktaba zenye vitabu,walimu wapewe mishahara na haki zao stahiki bila vikwazo hakuna mzazi au mlezi aache bure ampeleke mtoto private?tuache siasa ktk elimu na division za ajabu ajabu.Jemedari JPM hili kwako jepesi acha private watambe SHULE za serikali zikiwa bora private wataisoma namba

na huo ndio ukweli wanaoukimbia,ni wazi wanajua ila ni wavivu tu kuamua kufanya. Ziboreshwe shule za kina kayumba,hkn atakayeenda private. Ubishi tuhh,
 
Back
Top Bottom