kitindi1979
Member
- Dec 20, 2015
- 5
- 0
kazi ipo
TUME ya wataalamu waliokuwa wanakusanya maoni ya wadau wa elimu na kukokotoa ada elekezi kwa shule za msingi na sekondari zisizo za Serikali, wamemaliza kazi yao na tayari wamekabidhi ripoti hiyo kwa Serikali.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Sifuni Mchome amethibitisha kukamilika kwa kazi hiyo na sasa kinachofuata ni uchambuzi wa ripoti pamoja na kuangalia miongozo ya Serikali kabla ya ada elekezi kutangazwa na kuanza kutumika kwa majaribio mwakani Januari.
Wataalamu hao walipewa kazi na Serikali kuandaa ada elekezi baada ya kupata maoni ya wadau mbalimbali wa elimu wakiwemo wazazi, wananchi, wamiliki wa shule binafsi, walimu, asasi zisizokuwa za kiserikali, taasisi mbalimbali za umma na wadau wengine ambao wanaweza kusaidia katika ukokotoaji huo wa ada.
Katika ukokotoaji huo, wizara inaandaa mchanganuo wa gharama za kumsomesha mwanafunzi kuanzia elimu ya awali, darasa la kwanza hadi kidato cha sita kwa nia ya kutoa ada hiyo elekezi ambazo zitaendana na huduma itolewayo kwa shule zisizo za Serikali.
Alisema shule zitakazoteuliwa kuanza kutumika kwa ada hizo zitatangazwa pia na wizara hiyo baada ya kukutana na wamiliki wa shule hizo na kufanya nao mazungumzo.
Alisema majaribio hayo yatafanyika katika baadhi ya shule Tanzania nzima na sio katika baadhi ya mikoa tu.
....................................
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Sifuni Mchome amethibitisha kukamilika kwa kazi hiyo na sasa kinachofuata ni uchambuzi wa ripoti pamoja na kuangalia miongozo ya Serikali kabla ya ada elekezi kutangazwa na kuanza kutumika kwa majaribio mwakani Januari.
...............................Alisema shule zitakazoteuliwa kuanza kutumika kwa ada hizo zitatangazwa pia na wizara hiyo baada ya kukutana na wamiliki wa shule hizo na kufanya nao mazungumzo.
Alisema majaribio hayo yatafanyika katika baadhi ya shule Tanzania nzima na sio katika baadhi ya mikoa tu.
Kwa mtazamo wangu sidhani kama hili swala la karo elekezi linawezekana......kwani tution fee itakuwa ndogo.....ila ukiangalia gharama za maradhi na chakula sidhani kama hapo kunaweza kuwa na mjadala!!!!
Katika shule zilizo bora....mtoto anakula milo minne!! Anapata matunda,maziwa nk.....
Maradhi mtoto analala chumba kimoja watoto wawili.....bafu zuri na choo cha maji safi.......kwa mazingira kama haya ni bora kumuambia mwenye shule afunge shule afanye biashara nyingine........kinyume na hapo naamini haitawezekana.
Yaani kabisaaaaa.... ETI SHULE ZA SERIKALI ZOTE ELIMU BURE TOKA JANUARY 2016, LAKINI ZA BINAFSI BAADHI ADA ELEKEZI NA BAADHI ZITAACHWA NA MIADA YAO MIKUBWA..... Ipo namna
Hapo ulipoandika "gharama za maradhi" umenichekesha sana!!
Suluhisho ni serikali kuboresha shule zake. Hili likifanyika shule binafsi kwa aslimia kubwa watarekebisha ada zao.
Acha akili za kimaskini kupenda mteremko. Pambanakama mfumo hapa kazi tu wanaenda kujaribu nini? kinachotakiwa ni amri hawataki majengo wakafugie kuku.
hapa kidogo naona kama kasi ya MH Magufuli, inaelekea kupunguzwa na vigogo wenye shule hizi.
Ni ukweli usiopingika kwamba shule hizi zimekuwa mzigo mzito kwa walaji, gharama wanazotoza haziendani na uduma na ubora wa shule husika.
Majengo hovyo. Mazingira mabaya kabisa, njoo kwenye Ada ni kubwa sana, hapa serikali isipepese Macho itoe hamri moja full stop.
Mkuu nashukuru sana kuliona hili. Na kuna hili tatizo la "r" na "l" limekuwa kero.Hivi kizazi hiki mnafundishwa nini huko shuleni? pumbavu kabisa wewe, hiyo herufi "h" mbona unaifanyia ufisadi. ndio mnataka watoto wetu wakasome shule zinazofundisha hivi kiswahili?
Ni kweli mkuu, lakini ukumbuke hata kabla hawajasema elimu bure,Hakuna kitu kama elimu ya bure, inagharimiwa kwa kodi unazotoa serkalini. Kwa maana katika shule za serkali walimu wanalipwa mishahara, vitabu vinanunuliwa, huduma yote ya elimu inalipiwa gharama kubwa na hazina. hivyo ili na shule za binafsi kutoa elimu "bure" au kwa "ada ndongo sana" inabidi hazina ya serkali igharamie huduma hizi! Hapo elimu itakuwa bure!!!