PreGE2025 ACT Wazalendo yajipanga kushirikiana na Vyama vingine na Taasisi kupigania Uchaguzi Huru na Haki

PreGE2025 ACT Wazalendo yajipanga kushirikiana na Vyama vingine na Taasisi kupigania Uchaguzi Huru na Haki

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,436
Reaction score
5,230
Chama cha ACT Wazalendo kimesema kipo tayari kuunganisha nguvu na vyama vingine vya siasa pamoja na taasisi mbalimbali ili kuhakikisha vinapambania uwepo wa uchaguzi huru na haki mwaka huu.

Akizungumza leo Februari 23 kwenye Kikao cha Halmashauri Kuu ya chama hicho Kiongozi wa ACT Wazalendo Dorothy Semu amesema “Tukielekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, ni muhimu kutambua kwamba kuna hujuma na hila zinazotumiwa ili kukata tamaa wananchi.

Soma Pia: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Hali hii inatufanya tuwe na jukumu kubwa la kusukuma ajenda ya kuunda jukwaa la mapambano ya pamoja na vyama makini.”

Semu ameeleza kuwa umoja na vyama vingine ndiyo njia pekee ya kusaidia kuhakikisha upatikanaji wa haki kuelekea uchaguzi na kuzuia njia zote za hujuma dhidi ya vyama vya upinzani.

“Tunahitaji kufanya shughuli za pamoja ili kuimarisha umoja wetu wenye nguvu utakaoleta tija ya mabadiliko. Tunahitaji kupambania kuurejesha uchaguzi. Nchi yetu hasa hakuna uchaguzi. Tutaunganisha nguvu na vyama vyote makini na wadau wa demokrasia nchini.”

Snapinst.app_470914366_18097877950513179_9060112760217115370_n_1080.jpeg
Snapinst.app_480485790_18097877962513179_4715730682948793973_n_1080.jpeg
Snapinst.app_474078716_18097877971513179_6324729732342067769_n_1080.jpeg
 
JECHA alifutaga Ushindi

nitashangaa ACT kudhan kwamba Kwa uchaguzi uliopo wanaweza shinda Zanzibar .

ACT na CDM wakishaungana kwenye mapambano haya.

Hata CCM iwaahidi hao wengine Wabunge kumikumi, UCHAGUZI UTAKUA HAUNA MAANA.

NO REFORMS, NO ELECTION
 
JECHA alifutaga Ushindi

nitashangaa ACT kudhan kwamba Kwa uchaguzi uliopo wanaweza shinda Zanzibar .

ACT na CDM wakishaungana kwenye mapambano haya.

Hata CCM iwaahidi hao wengine Wabunge kumikumi, UCHAGUZI UTAKUA HAUNA MAANA.

NO REFORMS, NO ELECTION
Zitto Kabwe ni miongoni mwa watu wajinga waliokataa reforms na system overhaul! ccm ikatumia maoni yake kulete tume huru ya uchaguzi ambayo wajumbe wake wanateuliwa na Rais ambaye pia ni mgombea!
Shame on you Zitto!
 
Zitto Kabwe ni miongoni mwa watu wajinga waliokataa reforms na system overhaul! ccm ikatumia maoni yake kulete tume huru ya uchaguzi ambayo wajumbe wake wanateuliwa na Rais ambaye pia ni mgombea!
Shame on you Zitto!
Naunga mkono hoja zitto ni shushu wa chama tawala reform zote aliunga mkono sasa sijui kwanini alikuwa anaunga mkono ! Wanaotangaza matokeo ni wateule wa raisi na raisi mwenyewe ndiye mgombea pia raisi huyohuyo anaweza kumtengua mteule wake wakati wowote halafu wanakuja na jina la kinafiki tume huru ya uchaguzi ! Lini imekuwa huru sote tumeona uchaguzi wa serikali za mitaa ni upuuzi mtupu. Ni wakati wa no reform no election🔥🔥🔥🔥🔥
 
Wa
Chama cha ACT Wazalendo kimesema kipo tayari kuunganisha nguvu na vyama vingine vya siasa pamoja na taasisi mbalimbali ili kuhakikisha vinapambania uwepo wa uchaguzi huru na haki mwaka huu.

Akizungumza leo Februari 23 kwenye Kikao cha Halmashauri Kuu ya chama hicho Kiongozi wa ACT Wazalendo Dorothy Semu amesema “Tukielekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, ni muhimu kutambua kwamba kuna hujuma na hila zinazotumiwa ili kukata tamaa wananchi.

Soma Pia: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Hali hii inatufanya tuwe na jukumu kubwa la kusukuma ajenda ya kuunda jukwaa la mapambano ya pamoja na vyama makini.”

Semu ameeleza kuwa umoja na vyama vingine ndiyo njia pekee ya kusaidia kuhakikisha upatikanaji wa haki kuelekea uchaguzi na kuzuia njia zote za hujuma dhidi ya vyama vya upinzani.

“Tunahitaji kufanya shughuli za pamoja ili kuimarisha umoja wetu wenye nguvu utakaoleta tija ya mabadiliko. Tunahitaji kupambania kuurejesha uchaguzi. Nchi yetu hasa hakuna uchaguzi. Tutaunganisha nguvu na vyama vyote makini na wadau wa demokrasia nchini.”

 
✌️CHADEMA NA ACT WAZALENDO🤚 TUUNGANISHE NGUVU ILI KUPAMBANIA REFORMS BILA ONE FRONT HAWA CCM WATAENDELEA KUGOMEA REFORMS.
 
Back
Top Bottom