ACT Wazalendo pelekeni salamu CHADEMA

ACT Wazalendo pelekeni salamu CHADEMA

Unaona sasa!

Dada wenzio wanaotafuta wanaume wako kule jukwaa la MMU nenda kule kaanzishe uzi wadau watakufuata tu inbox.

Hii tabia ya kuvamia tu wanaume nlikuonya hutampata mtu.

Muuza CHIU wa ipogolo
 
Muuza CHIU wa ipogolo
Unaona sasa?

Usione aibu mkuu! Wewe nenda anzisha tu uzi wadau watamwagika huko Pm

Alafu kumbe ipogolo ndio kijiwe chako cha kuuzia nyapu?

Hongera dada
 
Napenda kumuambia rasmi kaka yangu Zitto Zuberi Ruyangwa Kabwe (Zizou Ziyaye Zinedine Yaziy Zidane) kuwa CCM hatunaga Shuguli ndogo. Kila uchaguzi kwetu ni muhimu na wathamani sana. Sisi siyo CHADEMA ambao wanakimbia uchaguzi mdogo wanashiriki uchaguzi Mkuu. Wakati Uchaguzi mdogo ndiyo unatafuta mabega ya kusimama wakati wa kueleka na kipindi cha uchaguzi Mkuu.

Zitto anashangaa WanaCCM kama Mh Kassim Majaliwa, Mh Dkt Mpango, Mh Shaka, Mh Cecil Mwambe, Mh Nyarandu n wengine kuwepo kwenye kampeni. Anashangaa haya kwasababu ya neno "UCHAGUZI MDOGO" ahhaa! Hilo ni jina tu kutokana na Wakati na kiwango cha Uchaguzi husika lakini thamani na maudhui yake kwa CCM ni UCHAGUZI MUHIMU.

Zitto Yeye hakuwatuma akina Ado Shaibu wala akina Likapo Bakari na Nondo Abdul bali alikwenda Yeye na Haji Duni kwani wenyewe ni wepesi kiasi hicho!? Namkumbusha kuwa Siasa ya Chaguzi kwetu sisi siyo ya kupuuzwa ni Kazi kazi tena kwa Jina la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Zitto ahakikishe anajenga chama kitaasisi wala asijiingize kwenye siasa za lawama, matukio na kutegemea CCM tukosee ndiyo watumia hiyo fulsa. Lazima wajikite kiajenda na kimuono wala siyo kijanjajanja kama wale jamaa wanaogombea Viti maalumu 19 tu.

Kigoma Tumeshinda kwa Kishindo kikubwa kwasababu Upinzani bado wanaleta na kuendekeza siasa za kivulana kuliko za kimajukumu.

Ukitaka kujua nguvu ya CCM basi jifanye unajaribu kuhatarisha Uhai wake... Chadema wanajua maana walishaingia ndani ya 18 hadi sasa wanaogopa kuingia ulingoni wamebaki kutafuta huruma ya Mama[emoji1787][emoji1787].

Tanzania bila CCM itayumba.
Acha kujisifia wakati tunajua rafu zenu. Ndiyo maana wenzenu CDM wamweka mpira kwapani. Nyinyi bila kufanya hivyo hampoati kitu. Ila Mungu yupo na siku moja yot yataisha haya, na sisi wengine tusio na vyama tutafaidi kwenye nchi yetu. Sasa hivi kuleni sana ubwabwa. Tunasubiri atakapokuja ambaye ataona muhimu ni watanzania kwanza kama Nyerere alivyokuwa anafanya. Pamoja na mapungufu ya Mwl Nyerere but he is the best leader and president we have ever had. Hawa wengine wachumia tumbo tu. Nyerere aliangalia maslahi ya watanzania kwanza. Ndiyo maana alijenga viwanda vingi sana na alianzisha mashirika mengi sana. Ajir ilikuwa kedekede. Hata daras la saba walitamba enzi zake. Waliajiriwa tu kwani viwandani huhitaji mtu wa vidato vya ajabu. Sasa hivi muda wenu wa lutamba lakini yana mwisho. Mungu ni wetu sote na anaona yote mnayofanya. Sisi kazi yetu kulilia tu na atatujibu tu!!!!!
 
Kule kuna kampeni za kuwania ukuu wa malaika na jamaa yenu yupo hoi kwa kukosa wapambe. Mbona hamuungi juhudi mkono?
Ha ha ha!!!! Ile ilikuwa blasphemy ya ajabu sana!!!!
 
Wananchi wamewapuuza ccm na uchaguzi kwa ujumla. Kundi kubwa la wananchi haliridhishwi na ccm tena, kwa ujumla ccm iko nje ya muda bila wao kujua. Ukitaka kujua ccm imechokwa usiangalie ushindi, bali angalia idadi ya wapiga kura. Kama idadi ya wapiga kura waliojiandikisha ni zaidi ya laki 3 sehemu zote kilipokuwa na uchaguzi leo, kisha wanatokea watu chini ya 50,000 hapo inabidi mjiulize. Ccm kwa sasa ni kama mwanafunzi anayepata division IV toka division I, lakini anajivunia kuwa wakwanza kwenye hiyo division IV! Kama mna akili na mnaamini mnakubalika, jiulize ni kwanini hamna wapiga kura kama zamani? Hebu weka idadi ya wapiga kura iliyojitokeza tujue inavyokubalika na sio kutangazwa washindi na tume yenu.
Wananchi wameshajua hakuna uchaguzi hapo ni danganya toto tu ndiyo maana tunaendelea na shughuli zetu. Waendelee tu lakini kila zama ina mwisho.
 
Kwahiyo nyie chadema mmepata division ngapi kwenye huo uchaguzi?
Mpaka sasa hivi CDM ina division 1. Kama utakumbuka tunavyomsifia mama wao walisema ni mapema sana kusifia. Tuangalie vitendo zaidi. nasi tukapause, hivyo tunasubiri tuone mama kama atayaishi hayo maneno yake. Na ndiyo maana CDM wakaweka mpira kwapani hadi hapo tume huru itakapopatikana.
 
Siyo dhalimu kama shetani ndiyo!

Je kitu gani kimefanya msishiriki uchaguzi mdogo? Au ndio mmeamua kumuunga mkono moja kwa moja?

Mifumo yote mibovu iko palepale. Tunataka tume huru ya uchaguzi. Isitoshe sio cdm tu hawajashiriki, bali ni vyama karibia vyote.
 
Hebu weka idadi ya wapiga kura ili tuone mnavyokubalika. Kama una bar yako na ulikuwa unauza crate 10 kwa siku, kisha sasa unauza crate 2, utakuwa mwendawazimu kujisifia kuwa unauza crate zaidi ya wengine wenye bar hapo mtaani kwako, bila kujiuliza wateja wameenda wapi na kwanini hawaji tena.

1621233957732.png
 
Mifumo yote mibovu iko palepale. Tunataka tume huru ya uchaguzi. Isitoshe sio cdm tu hawajashiriki, bali ni vyama karibia vyote.
Mnataka wewe na nani? Na unataka kupitia hapa jf?

Vyama vyote kama kipi na kipi?
 
Back
Top Bottom