Kuna taarifa za chinichini kwamba ATC wanakusudia kujiunga na UKAWA ili kuongeza nguvu ya upinzani dhidi ya CCM. Hii ni kwa sababu ACT wanaamini katika umoja na mshikamano na wanatambua kwamba UMOJA NI NGUVU. Nakumbuka siku Zitto alipozindua ACT alisema chama hiki hakina uadui na chama chochote. Nadhani alikuwa anajenga mazingira ya kutaka kuungana na UKAWA baadaye ili kuongeza nguvu katika safari ya kuelekea Magogoni.
MAONI YANGU
Kwa kuwa viongozi wa ACT wana chembechembe za usaliti, nawashauri UKAWA wasiwakubalie ACT kujiunga nao. Nina hofu huenda ACT wanatumiwa na CCM kutaka kuwavuruga UKAWA. Kuweni na hao wasaliti.
:israel:
Ukawa wanapaswa kufahamu kirusi cha usaliti kilichoko ACT hakina chanjo wala dawa. Wajihadhari sana.
Last edited by a moderator: