Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,987
- 20,271
Ninatamani sana siku moja watu wote tuwe na uoni sawa, ufikiri sawa, na uamuzi sawa. Bahati mbaya hilo halitawezekana chini ya jua aishipo bin-adamu. Hata katikati ya msitu wa wajinga, kamwe hawatawaza na kufikiri sawa.
Lakini ikiwa siku moja tutabahatika kujifunza kitu kinachoitwa lugha za siri, ama kwa lugha ya kitumwa zinaitwa "Code Language", basi tutaishi na kuidhibiti hila na uovu wote duniani,
Kwanini Jaji Mutungi anatumia code language ngumu kiasi hiki kwa jamii dhaifu? Mutungi anajua kwanini hili, bahati nzuri Zitto anajua kwanini hili. Furaha yangu ninamuona Zitto yule niliyetamani kumuona miaka mingi nyuma, Zitto yule anayezungumza lugha ngumu ya kiukombozi yenye mamlaka na kwa hakika ukitaka kumfaidi Zitto, msikilize akiwa amekwazika sanasana.
Act inafutwa, hawa hawatanii na hawajaribu, wako serious wamejiandaa kuifuta, Mutungi ndie aliyeisajiri ACT, anajua mtego ulipo, lakini Mutungi ndie anayeifuta ACT anajua vilevile mtego ulipo. Zitto anajua, Lucas Limbu anajua, Grayson M Nyakarungu anajua, Mwigamba anajua, Kitila Mkumbo anajua, Habib Mchange anajua, na wengine wanajua. Hawa wana kura ya veto. Kinachoitwa mashitaka katika barua hii ya Mutungi ni Code Language tu.
Anayeshughulikiwa sio ACT, bali ni Maalim Seif, hili mimi nililiona mapema kabla Maalim hajahamia ACT, nikatoa angalizo ambalo kimsingi nilitumia "Code Language" bahati mbaya wagumu hamkunielewa, na baada ya maalim kujiunga ACT nikatoa tahadhari kwa vyama vyote, nikitumia code language, vilevile sikueleweka kabisa nikaishia kutukanwa na kudhalilishwa. Lakini nilifurahi kabisa.
Kama ni sehemu muhimu ambayo Chadema tunatakiwa kuungana na ACT kwahakika nikuhakikisha tunazuia uhalifu huu, tukiruhusu ACT ifutwe, tumeruhusu Chadema ifutwe pia. Wale wahafidhina wenzangu wa Chadema tuvumiliane, twendeni kuitetea ACT, tukifanikiwa kuitetea ikasalimika, tutarudi kwenye siasa zetu za vyama.
Na Yericko Nyerere
Lakini ikiwa siku moja tutabahatika kujifunza kitu kinachoitwa lugha za siri, ama kwa lugha ya kitumwa zinaitwa "Code Language", basi tutaishi na kuidhibiti hila na uovu wote duniani,
Kwanini Jaji Mutungi anatumia code language ngumu kiasi hiki kwa jamii dhaifu? Mutungi anajua kwanini hili, bahati nzuri Zitto anajua kwanini hili. Furaha yangu ninamuona Zitto yule niliyetamani kumuona miaka mingi nyuma, Zitto yule anayezungumza lugha ngumu ya kiukombozi yenye mamlaka na kwa hakika ukitaka kumfaidi Zitto, msikilize akiwa amekwazika sanasana.
Act inafutwa, hawa hawatanii na hawajaribu, wako serious wamejiandaa kuifuta, Mutungi ndie aliyeisajiri ACT, anajua mtego ulipo, lakini Mutungi ndie anayeifuta ACT anajua vilevile mtego ulipo. Zitto anajua, Lucas Limbu anajua, Grayson M Nyakarungu anajua, Mwigamba anajua, Kitila Mkumbo anajua, Habib Mchange anajua, na wengine wanajua. Hawa wana kura ya veto. Kinachoitwa mashitaka katika barua hii ya Mutungi ni Code Language tu.
Anayeshughulikiwa sio ACT, bali ni Maalim Seif, hili mimi nililiona mapema kabla Maalim hajahamia ACT, nikatoa angalizo ambalo kimsingi nilitumia "Code Language" bahati mbaya wagumu hamkunielewa, na baada ya maalim kujiunga ACT nikatoa tahadhari kwa vyama vyote, nikitumia code language, vilevile sikueleweka kabisa nikaishia kutukanwa na kudhalilishwa. Lakini nilifurahi kabisa.
Kama ni sehemu muhimu ambayo Chadema tunatakiwa kuungana na ACT kwahakika nikuhakikisha tunazuia uhalifu huu, tukiruhusu ACT ifutwe, tumeruhusu Chadema ifutwe pia. Wale wahafidhina wenzangu wa Chadema tuvumiliane, twendeni kuitetea ACT, tukifanikiwa kuitetea ikasalimika, tutarudi kwenye siasa zetu za vyama.
Na Yericko Nyerere