ladyfurahia
JF-Expert Member
- May 10, 2011
- 14,758
- 9,589
Hay marafiki zangu;
natumai mu wazima wa afya na mnaendelea vyema na shughuli zenu na masomo kwa wale wanaosoma na biashara kwa wafanyabiashara, nawatakia kheri na fanaka naa ufanisi wa hali ya juu katika majukumu yenu
blue monday ya leo nimeonelea niongee nanyi jambo hili ambalo limenitatiza kichwani mwangu na nimeona nilitoe hapa kwenu wapendwa wangu,
wakati mwingine twajifunza vitu kwa kuona na kuiga. Na mambo mengine huwezi kufanya bila kuangalia umuhimu wa kitu unachotaka kukifanya kwa wakati huo, jamii ya sasa inajifunza vitu kwa kuona na kuiga mambo ya magharibi wanavyofanya, mpaka imepelekea kutothamini tamaduni na mila zetu. Vijana wengi wamejitumbukiza katika mambo ya kisasa na kuona hayo yanafaa na kumbe wanajidanganya wenyewe na kujiangamiza.
Hii hali ya watu, hususani vijana wengi kuiga mambo ambayo hayafai kabisa kwa jamii, wewe unangalia luninga hasa wanamuiziki wa majuu unaiga tembea, simama, uvvaaji wa nguo zao na hata kuongea pia siku hizi vijana wengi wanaiga mno, utakuta mtu kavaa nguo mpaka inasema utanidondosha chini yani iko chini ya makalio jamani kwanini lakini kwani kuvaa kawaida kutakuletea nini mpaka uvae hivyo.
Acheni kuiga fanya kile ambacho waweza fanya kwa mikono yako na nguvu zako
kwani unafikiri bill gate alimwiga nani kuanzisha microsoft ni ubunifu/ ugunduzi na kipawa alichopewa
na mungu kama nawe una kipawa/kipaji anza kukifanyia kazi usiige acha dhana ya kuiga haitakupeleka mbali mwishoe utabaki tu unashangaa na kuduwaa na mambo uliyoyaiga hayatafika mbali.
Fanya kwa uwezo na kipaji ulichonacho nawe utaona mafanikio
nawatakia siku njema na kazi njema
natumai mu wazima wa afya na mnaendelea vyema na shughuli zenu na masomo kwa wale wanaosoma na biashara kwa wafanyabiashara, nawatakia kheri na fanaka naa ufanisi wa hali ya juu katika majukumu yenu
blue monday ya leo nimeonelea niongee nanyi jambo hili ambalo limenitatiza kichwani mwangu na nimeona nilitoe hapa kwenu wapendwa wangu,
wakati mwingine twajifunza vitu kwa kuona na kuiga. Na mambo mengine huwezi kufanya bila kuangalia umuhimu wa kitu unachotaka kukifanya kwa wakati huo, jamii ya sasa inajifunza vitu kwa kuona na kuiga mambo ya magharibi wanavyofanya, mpaka imepelekea kutothamini tamaduni na mila zetu. Vijana wengi wamejitumbukiza katika mambo ya kisasa na kuona hayo yanafaa na kumbe wanajidanganya wenyewe na kujiangamiza.
Hii hali ya watu, hususani vijana wengi kuiga mambo ambayo hayafai kabisa kwa jamii, wewe unangalia luninga hasa wanamuiziki wa majuu unaiga tembea, simama, uvvaaji wa nguo zao na hata kuongea pia siku hizi vijana wengi wanaiga mno, utakuta mtu kavaa nguo mpaka inasema utanidondosha chini yani iko chini ya makalio jamani kwanini lakini kwani kuvaa kawaida kutakuletea nini mpaka uvae hivyo.
Acheni kuiga fanya kile ambacho waweza fanya kwa mikono yako na nguvu zako
kwani unafikiri bill gate alimwiga nani kuanzisha microsoft ni ubunifu/ ugunduzi na kipawa alichopewa
na mungu kama nawe una kipawa/kipaji anza kukifanyia kazi usiige acha dhana ya kuiga haitakupeleka mbali mwishoe utabaki tu unashangaa na kuduwaa na mambo uliyoyaiga hayatafika mbali.
Fanya kwa uwezo na kipaji ulichonacho nawe utaona mafanikio
nawatakia siku njema na kazi njema