Mwanaume wa namna hiyo alimuonea wivu mkewe kwa kubaki nyumbani wakati yeye akienda job
siku moja kamwambia Mungu, naomba na mm niwe mwanamke nienjoy kama mke wangu, maana mm daily nakonda yeye ananenepa.
Mungu akamwambia sawa, kesho ukiamka asubuhi utakuwa mwanamke naye mkeo atakuwa mwanaume.
Na ikawa hivyo.
yule jamaa (mke kwa sasa) akaamka kesho yake, akamwandalia mumewe chai akaenda job yeye akabaki anaandaa watoto na kuwapeleka shule,
kwa ufupi, ilifika mpaka jioni bado anahangaika na kazi za nyumbani bila mafanikio mpaka mume na watoto wakarudi hata msosi hakuna. wakati enzi zake alikuwa anakuta nyumba safi, watoto wasafi, na msosi tayari.....na wife msafi......
basi kufika usiku yuko hoi taabani, na mumewe anataka haki ya ndoa, akatoa kwa shingo upande huku akilalama uchovu.
Usiku wa manane akaamka na kumwambia Mungu, ni bora nirudi hali yangu ya uanaume maana naona kuwa mwanamke ni mateso zaidi ya nilivyofikiria awali. Mungu hana hiyana, akamwambia poa, utarudi kuwa mwanaume, ila ni baada ya MIEZI 9, maana ulipolala na mumeo umepata MIMBA.
ASANTE.