Abiria waliojeruhiwa katika ajali hufidiwa vipi?

Abiria waliojeruhiwa katika ajali hufidiwa vipi?

Kitaeleweka

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2012
Posts
394
Reaction score
88
Heshima kwenu!

Nilikua abiria katika basi na njiani tukapata ajali kwa kugongana na lori la mizigo ambapo madereva wote walikufa on the spot, mi nimejitibia kwa wiki 2 sasa nna nafuu naomba kujua hatua na taratibu za kufuata ili nilipwe stahili zangu na je vitu vyangu nilivyopoteza kama laptop na simu pia ntalipwa?

Gharama za matibabu na muda nliopoteza hospitali?

Naomba msaada wenu wanajamvi
 
Duh kwa hiyo nianze mwenyewe mdogomdogo? Ni shidaaaaaaa

Watakuzungusha sana, nakumbuka kuna kaka yangu aliwahi kupata ajali na basi ya Super Feo alikuwa anarokea Singida akapoteza laptop na vitu vyake vya mhimu,sasa si alikuwa katokea huko mbele amakuja TZ kufanya research. Bwana akataka kuleta habari za mbele akaenda kwa mwanasheria akapewa document akaenda NIKO insurance ndiko basi lilikuwa insured.Yaani kwa trip alizofanya NIKO Insurance ni sawa na ghalama ya kununua vitu vyake vilivopotea na mwisho wa siku hakufanikiwa chochote
 
Hiyo ni civil case muhimu uwe na risiti uliopewa ulipolipa nauli,loss report na pf3 unao uwezo wa kufungua kesi ya madai mahakani.unamshtaki mmiliki sio dreva.na watu huwa hawajui tu mwananchi anao uwezo wa kwenda mahakamani akafungua mashtaki kwa hakimu. muhimu ni risiti
 
Nenda kwenye ofisi za Super Feo na copy ya risiti, ripoti ya dakitari aliyekuwa akikutibu na gharama za matibabu yako. Mwenye gari wataangalia kwenye list ya wasafiri wa siku hiyo kama wewe ni mmoja wao na jina lako kama lipo. Zipo fomu za madai watakupatia kujaza. Hakikisha pia unaijua kampuni waliyokatia bima hi ni taadhari tu, kama wataleta mizengwe wasiliana na Tanzania Insurance Regulatory Authority.

Tanzania Insurance Regulatory Authority
 
Duh kwa hiyo nianze mwenyewe mdogomdogo? Ni shidaaaaaaa

Most of third party claimants do not know about their right and time required by insurance Act for the claims to be paid by insurer from the date of presenting a claim. The Act orders an insurer to settle claims within forty five days from the date of presenting a claim. In real practice insurers dealy paying claims within that time limit with no reasonable cause other that making third party to give up. Lack of awareness of third party leads it to be difficult for them to report to commissioner of insurance for legal action.

Insurance Act Sec 166 (1) "every person who acts in contravention of the provision of this Act commit an offence and shall where no punishment has been stipulated by any other section in this Act for that offence, on conviction be liable for not exceeds five million" Sec (2) "where an offence to which this section applies is committed by a body of persons, every director, manager, controller or principal officer of the company and every partner, manager or principal officer of the partnership shall be deemed to be guilty"

Public education should be given to people in order to report to the Authority any unreasonable delay of claims settlement.
 
Bwana Asante,umedanganya vibaya mno,siku 45 ni za kufanya payment na sio kusettle claim,nahisi km hiyo paragraph umecopy kutoka sehemu na kuja kupaste hapa,msidanganye watu,third party claims zinakuwa settled vizuri,tatizo linakuja third parties wengi wanajaribu kudanganya au wanakuwa na expectation za kiwango kikubwa cha malipo kuliko uhalisia na hili tatizo linatokana na sababu za kuwapo bush lawyers wengi mtaani,kwa mfano mleta uzi anaweza akafika kwenye kampuni ya Bima wakamwambia athibitishe kama alikuwa na laptop na akashindwa kuthibitisha,hapo utailaumu kampuni au mpeleka madai Kitaeleweka- kama unahitaji assistance nicheki nikuguide
 
Last edited by a moderator:
Kyemo mchango wako hausaidii jukwaa bali unavunja. Medal kwa uelewa wake kajenga hoja hiyo. Sasa wewe kama unaona anakosea sahihisha kwa kuonyesha njia sahii na sio kuponda tuuuuuuuu
 
Hivi unaweza kujenga hoja kwa kutoa information ambazo si sahihi?na pia sijaponda chochote nilichojaribu ni kuelewesha ndio maana nikamwambia mleta uzi km yupo serious,aonyeshe u-serious tumuonyeshe njia
 
Niko serious na ticket bahati nzuri haikupotea
Ajali ilitokea tarehe 30 july basi ni morobest ilikua inatoka mpwapwa kwenda dsm risiti ya laptop na simu I think nnazo nyumbani na vingine vyenye risiti pia huwa natunza zitakuwepo.
Hivi kama ela taslimu unathibisha vipi? Bank statement haitoshi coz nlidraw two days before the accident?
 
Bwana Asante,umedanganya vibaya mno,siku 45 ni za kufanya payment na sio kusettle claim,nahisi km hiyo paragraph umecopy kutoka sehemu na kuja kupaste hapa,msidanganye watu,third party claims zinakuwa settled vizuri,tatizo linakuja third parties wengi wanajaribu kudanganya au wanakuwa na expectation za kiwango kikubwa cha malipo kuliko uhalisia na hili tatizo linatokana na sababu za kuwapo bush lawyers wengi mtaani,kwa mfano mleta uzi anaweza akafika kwenye kampuni ya Bima wakamwambia athibitishe kama alikuwa na laptop na akashindwa kuthibitisha,hapo utailaumu kampuni au mpeleka madai Kitaeleweka- kama unahitaji assistance nicheki nikuguide

Kuna claimant mmoja anaidai Kampuni moja 200mil kisa alikatika mguu kwenye ajali fulani.

Je ana haki ya kudai hizo fedha??
 
Last edited by a moderator:
Inshu sio kuwa na haki ya kudai hyo pesa,inshu inathibitisha vp ili kulipwa hiyo amount
 
Km hzi kampuni zingekuwa zinalipa hizo pesa za kiasi hicho basi zisingekuwepo au mtu ungeombea upate ajali ili uukate
 
Kuna ambaye hata mmoja alishapata ajali akapata malipo? me naona ni theoretical kwamba ukiwa na risit nenda ofis za kampun utalipwa no such a hell, na utaenda kwa wanasheria kes itapigwa kalenda had ukate tamaa mwenyw, mwenye bas analipwa bas lake ww unaendelea kusota mahakaman, hii mambo ya malipo yanatakiwa ya simamiwe na chama cha kutetea abiria kama kipo
 
Kyemo nadhani kuna kitu unapaswa kufafanua kuhusiana na malipo ya bima .kwanza aina za bima na faida Zake kwa miliki wa chombo cha moto na abilia pili hatua za kuchukua endapo ajali imetokea. Hapo ndipo kuna tatizo. Kwa mfano mm ninamiliki gari ndogo na in a bima third party nimegongwa na daladala nimepata majeraha na kupoteza mali zangu Je bima ipi inapaswa kunilipa? Na ni hatua gani nizifuate niweze kulipwa. Bira shaka kwa kujibu swali hili utakuwa umetoa mwanga mzuri sio tu kwa abiria wahanga wa ajari bali pia kwa jamii kwa jumla .msaada wako tafadhali. .
 
Nafikiri hili swala linahitaji majibu zaidi. Watanzania wengi hatuna elimu ya hili jambo na tunapoteza haki zetu. Nasikia huko ulaya kampuni mpaka huwa zinafilisika kwa kulipa majeruhi na wafiwa...kwenye nchi yetu tunaweza kupunguza ajali kama tuki-practice hili maana wenye magari watakuwa makini ili wacje wakalipa gharama mpaka kufilisika kabisa
 
Back
Top Bottom