Abdallah Bulembo: James Mbatia hana shukrani

Abdallah Bulembo: James Mbatia hana shukrani

SUNGURA-MJANJA

JF-Expert Member
Joined
Mar 6, 2014
Posts
200
Reaction score
33
Jana m/kiti wa Jumuia ya wazazi Abdalla Bullembo alisema kuwa mhe James Mbatia hana shukrani kwasababu alikuwa na maisha magumu Mh. Rais akamteua kuwa mbunge na kupewa gari nzuri,anavaa suti nzuri lakini hana shukrani/heshima
kwa kitendo chake cha kujiunga na UKAWA na kupanda majukwaani kuiponda serikali ya CCM iliyompa ulaji.
 
Mhe Mbatia ameonesha mtu msomi maanake ni nini! Usomi wa kweli ni kuwa mtu mwenye mawazo na fikra huru na kutoa mawazo kwa faida ya taifa ni si kikundi au chama fulani. Taifa au nchi ni zaidi ya vyama na itikadi za watu au makundi. Kwake ubunge haikuwa zawadi binafsi na raisi alimteua kwa kuangalia uwezo na sio zawadi. Raisi Mhe Kikwete kwa kutumia madaraka aliyonayo kikatiba alimteua Mhe Mbatia kwa msingi huo huo wa kuipenda nchi yake zaidi ya siasa za vyama ni huu ushindi na sifa kwa raisi wetu kuiweka Tanzania mbele ktk uteuzi huu.

Pamoja na mapungufu ya raisi wetu kama binadamu yeyote, Mhe Kikwete amekuwa mfano wa kuigwa kulinganisha na makada wenzake kama Wasira, Bulembo na Kinana nk ndani ya CCM ambao mara nyingi siasa na kauli zao mara nyingi ni za kugawa watu kwa vyama badala ya kutuunganisha kama taifa kwani siku zote taifa ni namba moja.
 
Rais ni tasisi,ni nafasi inayoweza kufanya kazi na mtu yeyote bila kujali Itikadi.

Kupewa ubunge kwa Mbatia sio zawadi kama Kihiyo Bulembo anavyofikiri,na kama ni zawadi amwambie Rais amvue.
 
Mheshimiwa Rais alimteuwa akijua wazi kuwa ni mpinzani na si wakala wa CCM na inawezekana Rais lishauriwa hivyo na CCM ili kupunguza nguvu za CHADEMA na ndiyo maana data zote anazotumia anapewa na Serikali. Na mheshimiwa Mbatia angefanya tofauti na tabia yake ya awali asingeeleweka wala kuaminika na angjimaliza angali kijana kama alivyojimaliza mwenyewe Lyatonga mzee wa Kilalacha kwa ghiriba za CCM .
 
Naanza kupata mashaka na watu walio huko jumuia ya wazazi kama wako sawa kichwani au jumuia hiyo ni mkusanyiko wa watu wenye hitilafu ya fikra. Yupo na yule mwingine naye anaongea kabla ya kufikiri hapa JF.


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Wakuu, mwenye CV ya Bulembo naomba atuwekee tuweze kuangalia na hatimaye kujiridhisha juu ya uwezo wake wa kuchanganua mambo.
 
Naanza kupata mashaka na watu walio huko jumuia ya wazazi kama wako sawa kichwani au jumuia hiyo ni mkusanyiko wa watu wenye hitilafu ya fikra. Yupo na yule mwingine naye anaongea kabla ya kufikiri hapa JF.


Sent from my iPad using JamiiForums

Huyu Bulembo hajui hata Mambo ya Muungano ambayo yamependekezwa kwenye Rasimu ya katiba!

Alisikika akiwahadaa wananchi eti hiyo rasimu haijazungumzia afya, maji, elimu, kilimo nk!
 
Jana m/kiti wa Jumuia ya wazazi Abdalla Bullembo alisema kuwa mhe James Mbatia hana shukrani. kwa sababu alikuwa na maisha magumu Mhe Rais akamteua kuwa mbunge na kupewa gari nzuri,anavaa suti nzuri lakini hana shukrani/heshima kwa kitendo chake cha kujiunga na UKAWA na kupanda majukwaani kuiponda serikali ya CCM iliyompa ulaji.
Miongoni mwa watu wapumbavu huyu bwana ni miongoni mwao!!mara nyingi kauli zake uwa ni za ajabu!!
Uteuzi wa Mbatia ni kwa mujibu wa katiba,na katiba haijaweka masharti ya anayeteuliwa kuwa mbunge,hapa tatizo la Mbatia ni nini!!?tatizo kuna watu wanafikiri kuwa kuwa mwanasiasa ni lazima utetee kila kitu hata kama ni cha hovyo ilimradi tu ufurahishe upande wako,kwa akili hizi hata maendeleo ni ndoto,kamwe hakuna maendeleo bila mawazo tofauti.
 
Ina maana hawa vijana wa vyuo wanaojiunga tu CCM kwa ahadi za kupewa wali na fulana za kijani pindi wakijitambua wakaamua kuwa na misimamo tofauti na kuvua fulana za CCM watakuwa wamekosa shukrani?
 
Kama mlimchagua ili awe shukrani basi imeshakula kwenu!!
 
Jana m/kiti wa Jumuia ya wazazi Abdalla Bullembo alisema kuwa mhe James Mbatia hana shukrani. kwa sababu alikuwa na maisha magumu Mhe Rais akamteua kuwa mbunge na kupewa gari nzuri,anavaa suti nzuri lakini hana shukrani/heshima kwa kitendo chake cha kujiunga na UKAWA na kupanda majukwaani kuiponda serikali ya CCM iliyompa ulaji.

unazungumzia mabwabwa hapa
 
Mbatia anaipenda nchi kuliko siasa; huyu Bulembo ni mchumia tumbo ambae anatumika na magamba kama vuvuzela!!
 
Stupid Bulembo, ndiyo maana nchi haiendelei kumbe kuna baadhi ya viongozi bado ni mbumbumbu, kumbe bungeni kunatafsiriwa kuwa ni sehemu ya kutuliza maumivu na siyo mapambano
 
Abdallah Majura Bulembo HAJUI kusoma wala kuandika!Alikuwa kiongozi wa FAT (siku hizi TFF)wakati wa utawala wa Ndolanga na walipo badili katiba kuwa kiongozi wa TFF at least awe Form IV akaondoka!

Namjua jamaa huyu toka anauza mitumba na baadae bucha pale stand Musoma;kwake siasa ni kazi maana ndiyo mtaji wake!Bulembo atafanya nn CCM ikiondoka madarakani?
 
Back
Top Bottom