AAR na wizi wa mchana kweupeeee!!!

kadeco

Member
Oct 14, 2012
17
3
Kwa siku za hivi karibuni pamezuka wizi wa kuaminika unaofanywa na company ya bima ya afya iitwayo AAR. Kwa wale wafanyakazi ambao wanatibiwa chini ya company hii kwa kutumia kadi za waajiri wao wamekuwa wakibambikiziwa bill kubwa saana bila wao kutumia hiyo huduma au hailingani kabisa na huduma waliyopewa.
Wanafanikisha wizi huo kwa kukataa kujaza zile form za matibabu mbele ya mgonjwa na matokeo yake huzijaza wao wagonjwa wakishaondoka hivyo kupata muda mzuri wa kuchakachua wapendavyo.
Madhalani mtu ametiwa malaria kwa dozi wanayosema wao ni 15,000 lakini utashangaa bill inakuja ya 120,000 au hata zaidi.
Pia bill inakuja na makosa mengi ya ku justify wizi mfano kuonyesha umetiwa sehemu nyingi tofauti na pengine hujawahi kufika huko mfano mimi nipo Dar ila bill inaonyesha nilitibiwa mara 4 hospital moja ya mission ipo Arusha kumbe uongo mtupu mimi sijawai fika Arusha
Jamani hawa Wahindi wanatuibia sana.
Tukiona na kuchukulia simple wao wanaongeza juhudi za kutuibia na kupeleka mabilioni nje kama faida ya uwekezaji. Watanzania tutaibiwa hivi hadi lini?
 
Kadeco sidhani kama unajua hata namna bima za afya zinafavyofanya kazi.

Kama kuna uchakachuaji wowote hospitalini basi, anaibiwa bima na sio wewe, wewe unalipa premium ambayo ni around USD 800 or so kwa mwaka, baada ya hapo wewe unakua tu unaonyesha hiyo kadi na unapata matibabu, bili zote hulipwa na AAR, unless umepita kiwango ulichokua insured, na hadi hiyo itokee maanake wewe huwa unashinda tu hospitali.
 
Back
Top Bottom