A shameful battle field

A shameful battle field

Lukuvi aliuliza Makondakta ni nani katika serikali hii? Sasa yako wapi? Hapa tunamtaka waziri wa elimu atende haki! Hapa tunamtaka Rais wa JMT atende haki! Inaniuma sana ninavyomkumbuka rafiki yangu Mwl. Robert alivyotimua mbio kukwepa mkono wa sheria kutokana na kutumia cheti cha mtu mwingine kujipatia ajira mpaka akawa mwalimu mkuu!! RC naye aoneshe vyeti vya Bashite hapa! Na Paul Christian kule aliko anyamaze kabisa maana na yeye anaweza kuingia kwenye mkono wa sheria, bora ajikalie kimya ili siku akihitajiwa mahakamani akaseme alibiwa cheti chake!
 
Huku kwetu ya Makonda hayatuhusu.
Yanawahusu nyinyi wa kutwa kucha mitandaoni.
Na siamini kama mnafika hata robo yawatanzania
Mkuu umejiunga baada ya tuhuma za mkulu wako ili uje kuongeza nguvu za kutetea?...kama wanaomkosoa hawafiki robo kinachomliza ni nini?...Inaoenekana huguswi na hali ya watumishi makazini sasa ivi kwa matatizo haya haya ya vyeti...
 
KUSHINDWA VITA.

Mh. Paul Makonda ameshashindwa vita. Sio kosa lake kwa sababu ukienda vitani aidha kuna kupiga au kupigwa ndio maana kuna msemo " Backfire" ambayo inakuja kama KARMA ama LAANA au A COMPLETE DEFEAT na lazima ukubali matokeo na wapenzi wako wakubali kubaki kuwa wafariji wako na sio kukupa moyo eti, utayashinda yote kwa yeye akutiae nguvu kwani haiwezekani tena. Serikali imesema na sio Mh. Makonda akiwa mmoja wapo na sio Paul Makonda kasema ndiyo ilikuwa kigezo cha ushindi wa vita.


MAKOSA YA KIUFUNDI ALIYOYAFANYA MH. MAKONDA


1.0 LACK OF SITUATION ANALYSIS

Hakuna ubishi kwamba binadamu yeyote aliyefanikiwa kimaisha lazima awe amepitia milima na mabonde mengi. Kama ilivyo kwa Mh. Makonda, alipaswa kukumbuka alitokea wapi, yuko wapi na anaelekea wapi na hili halitegemei sheria, maandiko matakatifu wala kanuni zilizotungwa na kuhifadhiwa kimaandishi, isipokuwa utashi binafsi na ushauri wa kweli wa marafiki, ndugu na wanaofanya naye kazi ndio ilikuwa ngao yake ya kutekeleza majukumu akiamini kwamba kila analolitenda liko kisheria, limeamuliwa na wengi kwa kufuata mifumo sahihi ili kupunguza kasi ya kupingwa kama inavyoonekana sasa.


2.0 ALIKUWA KISIASA ZAIDI

Alitaka wateule wengine kama Kamanda Sirro, wakuu wa mikoa mingine, manaibu na mawaziri wao pamoja na makatibu wakuu waonekane wazembe wakati yeye akijijengea umaarufu, ili Mh. Rais amuone, amuamini na ampe majukumu zaidi ya aliyonayo ila kiuhalisia isingewezekana.


3.0 HAKUJUA VITA ALIYOTAKA KUPIGANA

Kuijua vita inahusisha kujiuliza maswali mengi pamoja na yafuatayo, Ni aina gani ya vita? , Ina maadui gani na uwezo wao kifedha na pia uwezo wao kiakili ni upi? Zaidi ya fedha na akili, maadui wana silaha gani za ziada? Je maadui wanayo political back-up be it national or international? Je kuna uzoefu wa kupambana na vita kama hii aidha nchini na au kimataifa? Je kama uzoefu upo, mbinu zipi zilitumika? Ushindi ulipatikana or it just ended as a lost war in the shameful battle field? Rasilimali watu, fedha na muda gani zitahitajika? Je technologia gani ya mawasiliano au ya mitambo/nyenzo za kivita zitumie hasa kwa kuzingatia technologia wanayotumia maadui?

Vita vitakapopigwana, madhara gani yategemewe? Na je ni kina nani wataathirika na kwa kiwango gani? Maadui wakiamua ku-counter attack, watatumia mbinu gani na mbinu zao zitakuwa na madhara gani? Anyway, so many questions to ask ila itoshe tu kujiuliza kwamba Mh. Paul Makonda amejiuliza maswali haya na mengine mengi? Mh. Makonda naamini utasoma hapa, je umegundua udhaufu wako hapa au utaishia kuniona mbaya kwa maoni yangu?


4.0 KUSHINDWA KUJITETEA

Mashambulizi yalivyozidi, Mh. Makonda alisahau nguvu ya dola aliyoitumia kwa cheo chake kuendesha vita na badala yake, akaanza kulalamika kuna mpango wa kutumiwa majini, mara kuonekana misikitini akiombewa na kanisani akilia machozi. Hapa ndipo what the scientist call " A Verifiable Indicator" of a no more strength to keep fighting but rather defending oneself.


SILAHA PEKEE

1.0 WANANCHI

Utashi wa watanzania waamue wamsamehe au waendelee kumshupalia japo kuna mgawanyiko hapa, wapo wanaomtetea na wanaomkosoa na inatokana na jinsi jamii ilivyoguswa na tuhuma zinazomkabili Mh. Paul Makonda ikilinganishwa na jinsi walivyomchukulia kabla hajatuhimiwa na uzito wa hadhi aliyonayo sasa. Kunyamaza kimya bila kujibizana na kina Gwajima ineemsaidia kupunguza msongo wa mawazo pamoja na mijadala mitandaoni pamoja na magazetini lakini sasa it is too late kwani kiuhalisia wakosoaji ni wengi kuliko wanaotetea.


2.0 UONGOZI WA NCHI

Hakuna njia nyingine zaidi ya aidha kumshauri Mh. Makonda ajiuzulu kwa heshima yake binafsi, familia yake, chama pamoja na serikali ama uteuzi wake utenguliwe ili mamlaka ya uteuzi ijijengee heshima ya utendaji kazi kwa haki hasa ukizingatia kuna waliopatikana na tuhuma kama au zinazofanana kwa kiasi fulani na za Mh. Paul Makonda ambazo madhara ya dhahama zilizowakumba zinaweza kuleta tafsiri ya uonevu pale makando kando ya Mh. Makonda yakipotezewa kiaina.


Nawasilisha
Who ever go to the equity must go with clean hands
 
Naguswa na nguvu kazi yataifa inayopotea kwa dawa za kulevya
 
Ila kwa uelewa wangu mdogo ni kwamba hakuna aina ya elimu inayohitajika ili kuteuliwa kuwa RC, nikikumbuka vizuri hata Baba wa taifa aliwahi kumteua Mkuu wa Mkoa wa Dar ambaye alikuwa Dereva Taxi pale Magomeni....Hivyo ningekuwa mimi ndo Mkuu wa Nchi hii, hakika nisinge Mwajibisha Mh. Makonda kwasababu hizo na ukizingatia kama kila ninalomuagiza anatekeleza basi huyo kwangu anafaa
 
Rationaliser kimsingi umefafanua kila jambo kwa hekima na busara sana. Shida ya yule dogo aliona njia nyeupe kwake kusonga mbele. Hakuuona hata utelezi alipokuwa akipita kwenye tope litokanalo na mvua. Hakujua kwamba kosa namba moja ilikuwa ni kumcharaza yule babu yake pale ubungo plaza. Hakujua kama hakuna adhabu mbaya kama itolewayo na Mungu pale muumizwaji anapo surrender hukumu ile kwa Mungu. Hata hivyo adhabu alokwishapata inamtosha. Ushauri wangu wa bure a jipe ujasiri wa ku confess tu. Watanzania ni watu wenye huruma sana watamsamehe tu. Ila akishasamehewa ajifunze
 
Endeleeni kutoa povu, na bahati mbaya watanzania wamewapuuza. Makonda anawalaza na viatu.
 
Mtoa mada anataka kuamnisha Taifa Viongozi wasipigane vita, Mtoa mada ameamnsha Taifa gwajima sio mtu mwenye makosa.....Mtoa mada anatujengea wananchi tuogope vita hata kama hatuna vifaa vya kisasa.....Wakat Eltrea wanapigana na Ethiopia ni wachache na walkuwa na silaha duni lakn waliwadunda vizuri tu....Makonda hajashindwa vita...Mako Vita vyake vinatokana na utendaji wake katika kazi.....wakat mtoa mada wataka mako hawekwe kando....Utajckiaje akiwa Naibu waziri??? Utahama Nchi? Wanaomshambuliwa Mako mitandaon hawafk hata theruth ya Watanzania...Ni kikundi kdg mno cha chadema na wauza unga.....
Wacha u naibu waziri mmfanye vice Presidwaa kabisa. Lakini vyeti mezani kwanza. Halafu inaonyesha ulivyo mbumbumbu wa sheria. Bila kuwa mbunge hawezi kuukwaa u naibu waziri. Labda ateuliwe kwenye ile nafasi ya mwisho iliyobaki. Otherwise itabidi kamanda Siro akusake kwa viroba. Sijui umevipata wapi?
 
Mtoa mada anataka kuamnisha Taifa Viongozi wasipigane vita, Mtoa mada ameamnsha Taifa gwajima sio mtu mwenye makosa.....Mtoa mada anatujengea wananchi tuogope vita hata kama hatuna vifaa vya kisasa.....Wakat Eltrea wanapigana na Ethiopia ni wachache na walkuwa na silaha duni lakn waliwadunda vizuri tu....Makonda hajashindwa vita...Mako Vita vyake vinatokana na utendaji wake katika kazi.....wakat mtoa mada wataka mako hawekwe kando....Utajckiaje akiwa Naibu waziri??? Utahama Nchi? Wanaomshambuliwa Mako mitandaon hawafk hata theruth ya Watanzania...Ni kikundi kdg mno cha chadema na wauza unga.....
Moja ya upumbavu ni kuchukulia kila mtu anaye taka ukweli uwekwe wazi dhidi ya tuhuma hizi za RC kuwa ni upinzani. Basi kama ni kweli,wapinzani wana hoja ya msingi kuliko wewe na wenzio team Lumumba.
 
Mange Kimambi kasema Maombi kwa rc ni sawa lkn yaelekezwe kwa nani?. Manake tuna Daud Bashite na Paul Makonda, na ktk maombi lazima utaje jina halisi la mlengwa. Rc taja jina uombewe nalo.
Inawezekana ndo maana vyeti havibadiliki majina. Wrong diagnosis wrong prescription
 
Huelewi hata kinachoongelewa.

Hawazungumzii ufaulu au kiwango cha elimu, hapa kinachoongelewa ni kukosa uaminifu, kughushi, kudanganya, na kisha kusoma kwa kutumia cheti kisichokuwa chake. Kama ni kweli, hii ni jinai.

Ila kwa uelewa wangu mdogo ni kwamba hakuna aina ya elimu inayohitajika ili kuteuliwa kuwa RC, nikikumbuka vizuri hata Baba wa taifa aliwahi kumteua Mkuu wa Mkoa wa Dar ambaye alikuwa Dereva Taxi pale Magomeni....Hivyo ningekuwa mimi ndo Mkuu wa Nchi hii, hakika nisinge Mwajibisha Mh. Makonda kwasababu hizo na ukizingatia kama kila ninalomuagiza anatekeleza basi huyo kwangu anafaa
 
Gazeti la mwanahalisi la leo ndio habari ya mjini. He can choose to give up or live in a great shame for the rest of his regime.
 
Back
Top Bottom