46 mbaroni kwa unyang'anyi, uharifu

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
266
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limewashikilia watuhumiwa 46 wa ujambazi ambao walikamatwa kwa makosa mbalimbali.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suileman Kova, alisema hayo na kufafanua katika eneo la Temeke askari walikamata silaha moja aina ya Brown iliyokuwa imehifadhiwa ndani ya jarida ikiwa na risasi mbili.

Mwananyamala polisi walifanikiwa kupata silaha na risasi za bunduki aina ya Rifle 73 zikiwa zimetupwa na majambazi baada ya purukushani kati ya polisi na majambazi hao.

Kituo cha mabasi cha Ubungo askari walifanikiwa kushika silaha aina ya SMG ikiwa imefungwa majarida matatu na ndani yake kukiwa na risasi 62.

Alisema silaha hiyo ilikuwa ikimilikiwa na abiria aliyekuwa akitokea mkoani Kigoma kuja jijini kwa lengo la kuungana na wenzake katika kufanya matukio ya ujambazi.

Mbali na majambazi hao, watuhumiwa wengine walioshikiliwa na jeshi hilo kwa makosa ya kuvunja nyumba za watu usiku na kuiba mali
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom