Dr Adam Francis
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 467
- 691
Unapo omba msamaha, ikukumbushe kuwa, waliokukosea katika makosa yao, nao wanastahili kusamehewa; usiwahukumu!
Unapo omba msaada, ikukumbushe pia wanaoshindwa, katika udhaifu wao wanastahili huruma; Usiwadharau!
Unapo omba kusitiriwa, ikukumbushe pia walio kwenye fedheha, katika aibu zao, nao wanastahili staha; usiwacheke!
Kupenda kusamehewa makosa yako bila kusamehe wengine, kupenda kuhurumiwa madhaifu yako bila kuhurumia wengine na kupenda kusitiriwa aibu yako bila kuwasitiri wenginge ni kizuizi kikubwa cha kupokea baraka kutoka kwa Mungu.
2026 nitawasamehe walionikosea, nitawahurumia walio dhaifu na nitazisitiri aibu za wengine wasipate fedheha.
SOMO: Mathayo 18:23-35
Unapo omba msaada, ikukumbushe pia wanaoshindwa, katika udhaifu wao wanastahili huruma; Usiwadharau!
Unapo omba kusitiriwa, ikukumbushe pia walio kwenye fedheha, katika aibu zao, nao wanastahili staha; usiwacheke!
Kupenda kusamehewa makosa yako bila kusamehe wengine, kupenda kuhurumiwa madhaifu yako bila kuhurumia wengine na kupenda kusitiriwa aibu yako bila kuwasitiri wenginge ni kizuizi kikubwa cha kupokea baraka kutoka kwa Mungu.
2026 nitawasamehe walionikosea, nitawahurumia walio dhaifu na nitazisitiri aibu za wengine wasipate fedheha.
SOMO: Mathayo 18:23-35