2025 tutawakataa wahuni na walipa visasi

2025 tutawakataa wahuni na walipa visasi

voicer

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2020
Posts
5,545
Reaction score
11,943
"Ni aibu mbunge anaposimama bungeni na kushangaa..eti ni kwa nini hakuna hata waziri wetu mmoja anayemiliki hata ndege moja nchini?" Je, kwa pato lipi kama sio kuusifia wizi,ufisafi na ubadhirifu wa pesa za walipa kodi wa Tanzania?

Ni kweli, tumekwisha yaona madhara ya wahuni ndani ya siasa na serikali,kupitia ripoti za CAG!
Hivyo ni wakati muafaka kuwakataa kwa vitendo,bila kumung'unya maneno!

Tumeyaona pia majigambo ya walipa visasi kupitia press release na vitabu uchwara vya vibaraka wao!
Ni wakati muafaka wa kuwakataa bila kuwaonea haya hawa mabaradhuli!

Na sasa tunayaishi madhara yao mitaani kwetu, kote nchini. Wananchi mnapaswa kujitetea kulingana na mnachokipitia,mkisubiri wasakatonge wa kisiasa,itakula kwenu milele!

Tumeisha yaona majigambo ya baba za wahuni mpaka kwenye vikao nyeti vya chama chao!
Wakijisifu kwa utamu wa kulamba asali,hadi wanaulizana...ni nani halambi asali kwa sasa?

Na kweli Hadi Ba*la amelambishwa asali na kuikacha ile klabu pendwa ya "visimbuzi" chezea asali wewe!

Na tunayaona madhara ya walamba asali kote mitaani kwetu! Amkeni hiyo 2025 myakatae hayo madhara kupitia vidole vyenu na midomo yenu,kwa kauli na vitendo!

Pamoja na kuitwa "mambuzi" na mgeni mualikwa kutoka Mesopotania! Bado mwenye kistuli wetu, aliwaamuru.."kila Mbuzi ale kwa urefu wa kamba yake!"

Na kweli wamekula urefu wao na kuumaliza,na mwenyekiti amekuja shtuka pale alipokuta wameingilia hadi karibu na bustani yake,ndio akajitahidi kuwaambia wahuni ...enyi "Stupid"

Ukweli ni kwamba neno stupid,lingesaidia kama lingetamkwa kabla hawajaiba,ila kwa sasa linakosa nguvu, maana wanalifurahia huku wakigongeana glasi za mvinyo wakati wakipongezana baada ya kuiba! (ushahidi ni ripoti ya CAG).

Wale mliopo kwenye fungate la asali kwa sasa,najua mtakalosema ila wananchi nao wanalo lao mioyoni ndani ya vifua vyao.

Tanzania sio mali ya koo fulani teule pekee,bali ilistahili kumnufaisha kila mtanzania kwa sababu hatukuchagua kuitwa watanzania!

Bali ni watanzania kwa sababu hapa ndipo tulipozaliwa kwa maamuzi yake mwenyezi Mungu. Na sio kwa hisani ya wanasiasa wasakatonge!

#Kataawahuni[emoji818][emoji419]
[emoji116]

IMG-20220829-WA0016.jpg
 
Mkuu!
Uzuri ni kwamba hivyo ilivyo inaeleweka pia!
sasa hivi inabidi kuandika kwa kupunguza ukali wa maneno sababu wahuni wanainekana kuwa na nguvu mpaka huku ndani ya platform!
Ban zinatembezwa kama njugu...hivyo .....
Hakika nimeluelewa
Watu wana hofu na KUANZA UPYA ndo maana wanahofia kuipiga chini CCM ambayo imefeli zaidi ya miaka 60 ya Uhuru.
Tulichobakia nacho ni kumshukuru Rais kwa kuamua nani apate maendeleo na nani akatishwe.....
 
Hakika nimeluelewa
Watu wana hofu na KUANZA UPYA ndo maana wanahofia kuipiga chini CCM ambayo imefeli zaidi ya miaka 60 ya Uhuru.
Tulichobakia nacho ni kumshukuru Rais kwa kuamua nani apate maendeleo na nani akatishwe.....
Ni kwamba ukiangalia bunge live,umegeuka ukumbi wa kusifia rais na kutafuta uteuzi!
 
Hivi kwann mnaogopa Sana kulipwa kisasi? Wakati mnawatendea wenzenu mliona raha Sana iweje sasa mnaogopa Sana kisasi?.

Acheni wazimu, Hao mliowatendea Ni binadamu wana mioyo ya nyama kama nyie.
 
Ni kwamba ukiangalia bunge live,umegeuka ukumbi wa kusifia rais na kutafuta uteuzi!
Kesi ya kubaka inaweza kumuweka mtuhumiwa jela maisha au miaka 30.

CCM ilibaka demokrasia nadhani kila ushahidi upo wazi na inatulazimu kumpiga ban ya maisha
 
Huez kua mwanaccm na upo ndan ya mfumo then useme CCM ni wahuni!! Kama CCM ni ya kihuni bas wote ni wahuni, cz hakuna alie msafi baada ya JKN. Tuwe wakwel bila ushabiki!!
 
Wahuni pia wamewaonea wafanyakazi sana wakati wa serikali ya awamu ya tano.
 
Ni kwamba ukiangalia bunge live,umegeuka ukumbi wa kusifia rais na kutafuta uteuzi!
Kuna kipindi bunge haikuwa ukumbi wa kusifia rais hapa Tanzania? Hiyo ni tamaduni ya Bunge la Tanzania kila nyakati...yote haya yanaletwa na wapuuzi wachache ndani ya nchi hii.
 
Back
Top Bottom