2015 yako ilikuaje,lets share,2016 umejipangaje

2015 yako ilikuaje,lets share,2016 umejipangaje

badiebey

JF-Expert Member
Joined
Nov 29, 2013
Posts
5,875
Reaction score
3,117
Hi wana Jf
Kama mjuavyo mwaka ndo unayoyoma kuisha hivoo.....msimu wa sikukuu mwaka ndo ushakata hivoo,
Leo tushare mwaka huu ulikuaje kwako,
Yapi mazuri,Yapi mabaya,ulipanga nini?umefanikiwa au la,kwa kiasi gani,na umejipangaje kwa next year 2016
Mie nashukuru kando ya shida nyingi za mahusiano,mwaka umeenda vzuri sana kifamilia, kikazi, kiafya na kiroho. Yani am happy so far, nilijitahidi kadri niwezavyo,Naamini 2016 ni bonge la mwaka kwangu Insha Allah,nmejipanga kwa mengi naamini yatatimia,
Wewe je??
 
Mwaka umekuwa mwema saaana kwa upande wangu, Namshukuru mungu paka hapa, na namuomba mungu siku zilizo baki ziende vema.

Nashukuru mwaka umekuwa mwema kwa vile nimempata nmpendae pamoja na changamoto nyingi mnoo, Nmemaliza masomo salama...

2016 Mungu anibariki nitimize malengo.....
 
Mwaka ulitaka kuisha vibaya kwangu baada ya jembe langu LOWASSA kutoingia mjengoni...
siyo mbaya lakini kwasababu Mr.JPM anafanya kile tulichokitaka[ila nasikia ana nyodo sijui ndiyo kalewa sifa?]

all in all,Mwaka unaisha vizuri kwangu..! welcome 2016
 
Mwaka unaisha poa Allah atujalie tumalize salama
 
Kwangu Mwaka unakwenda kumalzika poa sana kwa asilimia kubwa mambo niliyo panga kuyatimiza 2015 nimeyatimiza.
jambo moja tu limeniangusha mwaka huu 2015 "tumeachana na mchumba wangu mwezi wa sita" kwahyo ratiba yang 2016 ntaanza na kuanzisha uchumba mpya.
 
kwangu mwaka kwa ujumla ulikua mzuri malengo makuu yametimia kwa kiasi kikubwa namshukuru Mungu i hope 2016 Mola atajalia zaidi, disappointment kubwa kwa mwaka huu ilikuwa ni lowassa kushindwa urais!
 
Namshukuru sana mungu wakati naingia mwaka 2015 nilimuomba mungu anitimizie mambo matatu na yote nimefanikiwa ingawa si kwa aslimia 100. 2016 kwangu ni mwaka wa mabadiliko naomba mungu anisimamie nitimize tena malengo yangu
 
Huu mwaka ulianza vizuri kwangu ila hapo kati mwaka ukanikalia kichwa chini miguu juu....ila kwa yote nashukuru Mungu, hopefully 2016 utakua poa sana
 
Huu mwaka ulianza vizuri kwangu ila hapo kati mwaka ukanikalia kichwa chini miguu juu....ila kwa yote nashukuru Mungu, hopefully 2016 utakua poa sana

Miss yuuu,utakua poa ucjali mami
 
2015 ulikuwa mbaya sana kwangu, nmepitia nyakati ngum sana kimahusiano, nmepata na kupoteza!!
kikazi pia nmepata majaribu sana na kila nilichokichuma hakikukaa wala kuzaa!!

Mwisho WA mwaka nmegundua yooote yalikuwa mtaji kwa MWAKA 2016!!
Nmejifunza na kugraduate PhD ya mapenzi this year!
next year nitakuwa part timer vyuo vichache adi ntapopata wngu wa maisha!!
 
Mwaka huu ulikaa kushoto
sikutegemea a lot...
naona mwakani nitamaliza unfinished business
 
Baada ya mwaka mpya ndio ntatoa conclusion,still have some to finish up
 
Lengo kuu kwangu mwaka huu ulikuwa ni kuoa....nashukuru Mungu nmetimiza nmefunga ndoa..

next year,, nna malengo mkuu mawili.
1: Kuanzisha mradi/biashara kwa ajili ya familia yangu
2: kununua kiwanja na kuanza ujenzi mdogomdogo..

Kwake yeye kila jambo linawezekana....Mungu Mkuu
 
Mwaka Jana ulikua mwaka was majanga makubwa sana kwangu, nilipoteza kazi, niliugua, ila mwaka huu Mungu amenifuta machozi, nimeanzisha biashara, nimepata kaz mpya na nimeoa
 
mwaka 2015 ni mwaka wa mabadiliko makubwa kwenye maisha yangu..

niliacha kazi after 4 yrs na kwenda kusimamia kikampuni changu.. nilikuwa kila siku nasogeza mbele kuacha kazi but june 2015 nikafanya maamuz magumu.. thanks a lot kwa mama watoto wangu kwa kupush nikajarib my talent outside.. niache mipango ya ndotoni tu

namshukuru sana Mungu sana kwa dealz nilizozipata this year.. kazini nilipoteza sana muda na uoga wangu ulinirudisha sana nyuma...

nina imani 2016 utakuwa mwaka mzuri na zaidi na zaidi...
 
Alhamdulillah baada ya kuchukuwa miaka mitano kuzunguka sehemu nyingi Duniani nimekamilisha Safari ya Hijja 2015 !!!
In~shaa~Allah Mwaka 2016 nitakuwa katika upanuzi wa network kimataifa niliyoanzisha.....
Eee Mwenyezzi Mungu nisaidie.. Allahuma AMIN
 
Namshukuru Mungu mimu ni mzima wa afya pamoja na familia yangu..
Nimepitia mengi sana hadi nikajikuta nimejiunga huku
Ila Mungu ni mwema natumain next year utakuwa mwaka wa rehema
 
Nilitaka kuacha pombe lakini mpaka sasa zimebaki week mbili sijafanikiwa katika hilo. Hope mwakani mambo yatakuwa safi...
 
Back
Top Bottom