Hapo kwenye ku-carry cash.
Siku moja rafiki yangu wa kike aliniita sehem tukale bata. Mimi na huyu dada tulikuwa tushatengeneza kama ki desturi flani hivi. Yule atakeye mwalika mwenzie, ndiye atalipia bills zote za mtoko. Hatukuwahi kusemezana hivo ila ilitokea tuu ikawa hivo.
Siku hiyo ilikuwa weekend. ndo najiandaa kulala, akanipigia simu...njoo mahala fulani kuna karaoke. Nikaona isiwe tabu. Nikamtimbia. Sikubeba cash.
Nafika nakuta kwenye meza yupo yeye, mdogoake wa kike na njemba Siijui. Nikajisikia vibaya ghafla. nikawaza inamaana kaniita mimi nilishwe bata na bwanaake!!!.. nikawapa hi. Halafu nikakaa kinyonge. Akaniambia niagize nnachotaka. Sikuagiza. Nadhani aligundua nimekua disappointed.
Haikupita hata dakika, nikamwambia nakuja, huku nanyanyuka kuondoka. nikachukua boda chap akanipele ATM nikavuta mpunga kama kilo mbili hivi. Moyoni najisemea kama yule mwamba ndo kaorganise mtoko, stumii senti yake. Nitaagiza vyangu na nitajilipia.
Nilikuja kucheki simu nikakuta kantext 'Just come back. I dont even know this guy. Katuvami tuu hapa'. lakini pamoja na i dont know this guy nilisema tuu ni lazima niwe na cash mfukoni aisee.