"Tunataka kuona katika Taifa hili, vijana jeuri na wenye kujiamini, si vijana waoga, akina "ndiyo bwana mkubwa", vijana wanaohoji na kupiga vita mifumo ya jamii isiyoshabihiana na matakwa na matarajio ya jamii ya kitanzania. Tunataka vijana waasi dhidi ya mifumo kandamizi, ubwana na ufisadi...
Maendeleo na mabadiliko ya Babati yataletwa na kijana wa Babati ambaye anajua ni nini wanababati wamekosa kwa muda mrefu. Pamoja na kuwa anafanya kazi Babati mjini pia ni kijana mzalendo na anayeshirikiana na wananchi katika maisha ya kila siku. Mtu kama huyo ndio anayehitajika na anayetafutwa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.