Mwaka 2021 wakati Rais Samia anaingia madarakani, Uzalishaji wa korosho ulifikia Tani 216,907 zilizoiingizia Tanzania $181M sawa na TZS452.5bn.
Mwaka 2024/25 Tani 528,260 zilizalishwa na thamani yake ni $600M sawa na TZS 1.6Trilioni.
Chini ya Rais Samia Mapato haya ya Korosho yameongezeka...
Msanii wa Bongo Fleva ambaye pia ni Mtangazaji wa Wasafi FM, Clayton Revocatus Chipando maarufu kama Baba Levo, na mtia nia Ubunge Jimbo la Kigoma mjini Kupitia CCM, amekea vikali kauli za Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe aliyoitoa kuwa Wasanii, Wachekeshaji na Watangazaji sio watu sahihi...
Naongea haya kwa masikitiko makubwa
Moja ya watu waliotuhumiwa kwa utekaji na Mambo mengine moja wapo ni Hawa watu
Halafu leo wanagombea Tena ubunge na nchi hii ilivyo ya mazuzu wanawashangilia tu
Hawa watu WANATAKIWA kukamatwa na takukuru na kohojiwa kwanza kwa kutumia madaraka yao vibaya...
Mkuu wa Mahusiano ya Kimkakati Clouds Media na Mchambuzi nguli wa habari za michezo nchini Shaffi Dauda ‘Digala’ leo tarehe 30 Juni , 2025 amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa na Chama cha Mapinduzi CCM kuwania Ubunge jimbo la Temeke
Mwanasiasa Fadhili Fabian Ngajilo rasmi amechukua fomu ya kugombea ubunge wa Jimbo la Iringa Mjini kwa mara ya tatu kupitia chama cha Mapinduzi (CCM).
Akizungumza na waandishi wa habari Ngajilo baada ya kuchukua fomu hiyo kwenye ofisi kuu ya ccm wilaya ya iringa mjini amekishukuru chama cha...
Kinyang’anyiro cha Ubunge wa Viti Maalum kundi la Vijana kinaendelea kukolea moto baada ya Monalisa Daniel, Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Taifa (UVCCM), kuchukua fomu ya kuwania ubunge wa Viti Maalum kupitia UVCCM.
Monalisa ambaye amejijenga na kukubalika na...
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA.
Awahakikishia viongozi wa dini, taasisi za kijamii na kimila
Awapongeza wanawake kusimamia amani
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amesema kuwa maoni yoyote yanayolenga kuhakikisha...
Sasa hivi kila jimbo la uchaguzi wanaCCM wanavutana nani awe Mbunge wao. Vijembe na mikwaruzano imeanza kutokea
WanaCCM watauana safari hii sababu ya ubunge na udiwani.
Wakuu, kama kichwa kinavyosema, toka mwaka uanze mpaka leo hii June 13 umeona gari la kuzoa taka mara ngapi mtaani kwako?
Kwakweli toka mwaka huu uanze Mtaani kwangu kule Mbezi Beach sijaona gari la taka hata mara moja. Kwa wanaozalisha taka ndogo huwa zinachomwa tu na zile za kuoza zinawekwa...
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule ametangaza kuwa maadhimisho ya Siku ya Samia mwaka huu yatakuwa ya kipekee na ya kitofauti.
Amesema kesho Juni 3, 2025, badala ya kukusanya watu wote ukumbini kama walivyokuwa wanafanya, kwa kesho siku hiyo itaadhimishwa kila kata katika Mkoa wa Dodoma...
Wakuu,
Akiwa anazungumza leo kwenye uzinduzi wa Ilani ya CCM 2025 ameonya wale watu ambao wanaenda majimboni na kuanza kusema kuwa wametumwa na Rais Samia pamoja na Mwinyi ili waweze kupitishwa na wajumbe kama wagombea wa CCM.
Rais Samia amesema kuwa yeye na Mwinyi hawajatatuma mtu yeyeote...
Ndugu zangu Watanzania,
Ningependa Kuwaambieni na kuwakumbusheni Ya Kuwa Pamoja na Katiba yetu kuwa wazi na kunyooka kabisa juu ya nini kinapaswa kufanyika pale Rais aliyepo madarakani anapofariki Dunia, Yaani Makamu wa Rais Kuapishwa na kuchukua Madaraka ya Urais kuongoza Nchi.
Lakini ni...
Yani bado wabunge wanatuchukulia poa kiasi hiki?
===
Mbunge wa Jimbo la Buchosa, Eric Shigongo, amewaeleza wananchi wa kata ya Illigamba kuwa tayari ameagiza vifaa vyake binafsi kwa ajili ya kutengeneza barabara katika maeneo mbalimbali ya jimbo hilo.
Akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika...
Ujenzi wa barabara ya mzunguko wa nje ya Jiji la Dodoma (ring road) umefikia zaidi ya asilimia 85 ya utekelezaji wake.
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amesomewa taarifa hiyo alipotembelea ujenzi huo ili kuona maendeleo yake.
Barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 112.3, ni miongoni mwa...
Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) kimetangaza kuwa kitaanza oparesheni maalum ijulikanayo kama C4C Tusonge Mbele kuanzia Mei 30, 2025 jijini Mwanza, kwa lengo la kuwafikia wananchi wa mikoa yote ya Tanzania ndani ya siku 16 kwa kutumia usafiri wa helikopta (chopa).
Tangazo hilo limetolewa na...
Hawa makada wa CHADEMA niliowataja ni vigumu mnoo kuendelea kuwa wanachama wapigania mabadiliko ndani ya CHADEMA hii ya msimamo mkali wa kisiasa.
Ni suala la muda tu.
Kuna ambao wangetaka kuondoka wakati huu pia, ila mfumo unawabakiza hili kujua mipango na mikakati ya CHADEMA hasa wakati huu...
Tako jana majeshi ya Israel yalikuwa yakitoa maelekezo kwa raia wa Gaza kutulia ndani ya majumba/Mahema yao huku wakisubiri maagizo mengine kutoka ngapi za juu za majeshi ya Israel.
Mchana wa leo hii Majeshi ya Israel yametoa amri raia wema waondoke maeneo hayo waelekee kaskazini mwa Gaza na...
Wakuu,
Hivi sheria zinasemaje kuhusu hizi plate number za kwenye magari?
Ni kwamba mimi naweza tu kuamka asubuhi nikaweka jina lolote as plate number au kuna muongozo ambao inabidi ufuatwe?
Vipi kwenye plate number nikaweka maneno yanayozua taharuki au nikaweka jina la mgombea Urais hasa...
Leo hii, kama vyama vyote vya siasa vingechukua msimamo wa kukataa kutia sahihi kanuni za uchaguzi, amini nawaambieni, sasa hivi tungekuwa tunaongea mambo mengine kabisa. Vyama vya siasa havikuiona na kutambua kuwa hiyo ilikuwa nafasi ya kuilazimisha CCM kukaa nao mezani na hata kubadili kanuni...
Haya ndio madhara ya Bunge na Serikali vyote kutoka kwenye chama kimoja. Yaani hizi kamati za Bunge kazi yake imekuwa ni kupongeza tu. Sijawahi kuona hata mradi mmoja ambao hizi kamati zimesema kama hauendi vizuri.
Tukisema hizi ni kampeni za Uchaguzi mtakataa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.