Elections 2015 Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) yafuta Matokeo yote ya Uchaguzi Mkuu

JamiiForums

JF Official Account
Nov 9, 2006
6,202
5,012
Katika hali ya kushtua Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar(ZEC) imetangaza kuyafuta Matokeo ya urais wa Zanzibar.

Yadaiwa Uchaguzi uligubikwa na kasoro nyingi.

Imeahidi kutangaza tarehe rasmi ya kurudiwa uchaguzi.

====
Statement:

vU05dG9.jpg

EdIidYV.jpg

BLhdlD9.jpg


VIDEO:

Chanzo: ZBC TV
 
Last edited by a moderator:
Hatimaye ZEC wamefitilia mbali uchaguzi wa Zanzibar.

Kwa mujibu wa tangazo la ZEC wameainisha mambo mawili ambayo yamepelekea kufutwa kwa uchaguzi huo ambayo ni mgombea mmoja kujitangaza mshindi kinyume cha taratibu na jambo lingine wamedai kuwa uchaguzi huo haukuwa wa huru na haki.
 
Duuuu.....ni kweli wakuu.
Tamko la kufutwa matokeo hili hapa

151028110039_zanzibar_640x360_bbc_nocredit.jpg



Je, nchi itakuwa chini ya nani kama Rais,....??
kwani katiba inasemaje kuhusu ukomo wa utawala hapa Zenji..??
ufafanuzi tafadhari.
 
sasa ndo wataumia zaidi katika hii raundi ya pili.
Leo mpatanishi wa mataifa mengine yamemfika shingoni.
sijui ni nani atayemuokoa na hili dubwana linalo mnyemelea.
 
Mwenyekiti wa ZEC amesema uchaguzi ulikuwa na kasoro nyingi, hivyo kwa mamlaka
aliyokuwa nayo amefuta matokeo yote ya uchaguzi Zanzibar. Uchaguzi kurudiwa tena.
Taarifa zaidi zinafuata
 
Back
Top Bottom