Hivi ni Trump anayeuwa au sheria imeamuru hivyo? Kwa hiyo wewe ukiwa rais utaacha kufuata sheria? Kwani rais ndiye aliyetunga sheria hiyo? Watu wenye akili ndogo hujadili watu, wenye akili za wastani hujadili matukio, bali wenye akili nyingi hujadili dhana.
Baada ya Marekani kupata uhuru July 1776 toka kwa Mwingereza, Wamarekani weusi wakajikuta kumbe uhuru ni wa weupe. Ndipo Henry, Mmarekani Mweusi, mwanaharakati, alitamka maneno hayo hapo juu.
Kwa tafsir isiyo rasmi: "Je, uhai ni muhimu sana, au amani ni tamu sana, hata kwa gharama ya minyororo...
Wanafunzi tunapenda A's badala ya maarifa kichwani! What a tragedy to the nation! Ukipata kazi wazazi wanapenda mafanikio makubwa ndani ya muda mfupi bila kujali kipato cha watoto wao! Immoral people or barbarians!
Maamuzi yanakuwa mepesi iwapo nchi au taasisi inaendeshwa kwa kufuata misingi ya sheria na kanuni walizojiwekea wenyewe. Lakini hilo linaonekana kufutika kutokana na kauli yako mwenyewe: "Kuna watu wazito nyuma ya akina Halima na wenzake."
Kama tunavyoshuhudia uvunjifu mkubwa wa katiba na...
Mnapobaini mmepote porini na Kiongozi Mkuu wa safari hajali kabisa kuangalia ramani yenu (the constitution) au compass ya kuonesha North (sheria na kanuni mbalimbali za nchi) ujue mtasota sana porini, na pengine kuliwa na wanyama au kupotea zaidi.
Watunga sheria na watoa maamuzi wetu...
Mfalme Sulemani, anayesadikiwa kujaliwa akili nyingi kuliko watawala wote waliowahi kuishi alisema, "Mwenye kutawala akisikiliza uongo; Basi watumishi wake wote watakuwa waovu." Mithali 29:12.
Lakini Petro na mitume walipoamuriwa kwa nguvu na baraza (Sanhedrin) wasihubiri tena kwa jina la Yesu walisema, "...Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu" (Matendo 5:29).
Naam, tunaamuriwa kuwatii wenye mamlaka kwa kuzingatia haki ya Mungu, lakini si katika maovu. Maana mwenye mamlaka juu ya...
Ushahidi kutoka kwa msimamizi mkuu wa kituo fulani (jina linahifadhiwa) anasema, "Nilitafuta makada wa CCM kama mawakala wa vyama vya siasa vingine, maana vyama vingi havikuweka mawakala katika vituo. Kwa hiyo, walioapishwa kama mawakala wa vyama vingine ukiwaondoa wa Chadema, hawakuwa mawakala...
Wanataka watawale kila kitu chetu, hata maoni yetu! Hawa ni zaidi ya Mungu katika maisha yetu. Mungu ameturuhusu kusema na kuwaza chochote, lakini si serikali hii.
Katika historia hakuna utawala wa kibinadamu ulidumu milele, hakuna! Kwanini sisi tudhani ni baghairi (exceptional)? Nithibitishe hoja yangu kwa mifano michache ya mataifa makubwa yaliyowahi kutawala dunia, lakini yaliangukia pua:
(1) Babeli, chini ya Nebukadneza, iliyashinda mataifa makubwa...
Naona Shetani anatamani chuki baina yetu Watanzania izidi kushika kasi. Historia haijawahi kuwadanganya wanadamu. Ni mkweli sana. Hata sisi tunaojibainisha kuwa "kisiwa cha amani" kwa miongo taktibani sita sasa tangu uhuru, tutaja shangaa, tukikataa kujifunza ukweli wa historia. Wakati mwingine...
Hoja zako ziko kwenye "deductive and inductive ways of thinking." Je, ni kweli wachaga wote ni wezi? Si kweli.
(INDUCTIVELY)
A: Ambwene ni Mnyakyusa.
B: Ambwene ni mgomvi.
C: Kwa hiyo, wanyakyusa ni wagomvi.
AU (DEDUCTIVELY)
A: Wanyakyusa ni wagomvi.
B: Wewe ni mnyakyusa.
C: Basi wewe ni mgomvi.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.