Nasikitika sana kueleza kuwa Kitengo cha Huduma kwa Mteja au Customer Care FASTJET hakitoi hutuma bora kwa wateja. Leo nimepiga simu yao na ikapokelewa lakini majibu niliyokuwa napewa na Mhudumu (Binti) sio kabisa. Anaongea kama kalazimishwa na anakuwa mkali kama vile anaongea na houseboy wake...
Ni mtazamo wako ndugu. Kila mtu kajaliwa ubongo wake. Kuna wanao ona mambo kwa upeo mpana hawa wanaitwa Great Thinkers na pia kuna Myopic minds ambazo wao hufikiri juu juu tu. Sikuchagulii kundi ila tafakari.
Sina lengo la kutafuta umaarufu kwa kumzungumzia mtu ambaye kwa sasa anaonekana kuwa maarufu zaidi nchini Tanzania. Ana mvuto wa pekee na kajijengea heshima kubwa katika jamii. Anakubalika kila eneo. Bara na Visiwani; Wakristo na Waislamu, Wenye kumcha Mungu na Wapagani; Wazee na Vijana; Wanaume...
Vyovyote itakavyokuwa, ningefurahi kumwona Bungeni Mama yetu Mpendwa sana Regina Lowassa. Ninaomba sana Mhe. Mbowe vile viti maalum vya Ubunge wa Kuteuliwa, tafadhali sana kimojawapo apewe mama yetu Regina. Endapo Mhe. Lowassa akishinda kiti cha Urais hiyo itakuwa habari nyingine.
Nina kila...
Vyovyote itakavyokuwa nadhani kesho LOWASA atakuwa na Mkutano wa Kihistoria kwa Jiji la Dar es Salaam. Hili lipo wazi, kwa namna yeyote kesho nguvu ya Edward itadhihilika na kuwatetemesha sana mahasimu wake kisiasa. Kila la heri CCM na mkutano wenu wa leo hapo Jangwani.
Ninapenda niwashukuru kwa michango mizuri ambayo mmeendelea kuiweka katika Mada hii. Nimepitia michango yenu yote ambayo mingi inalenga kuboresha zaidi. Ninakubaliana kabisa kuhusu uwepo wa WIZARA YA MAMBO YA NJE. Nadhani hii sasa itafanya Wizara zifike 16. Hatuna sababu yeyote ya kuwa na...
Punjab; Wizara ya Michezo, Utamaduni na Sanaa (Of course nimeambiwa tuongeze na Habari) ni muhimu sana. Hii ndio yenye kutambulisha utaifa wetu. Taifa lisilokuwa na utamaduni wake na kuuenzi ni sawa na taifa MFU. Nadhani ipo haja ya kuendelea kuwa na Wizara hii.
Habari yenu Watanzania wenzangu,
Kila jambo na wakati wake kwa majira yake. Uchaguzi Mkuu unafanyika Oktoba, 2015 siku ya Jumapili. Si rahisi kubashiri nani ataibuka mshindi katika kinyang'anyiro cha Urais pengine tusubiri kuona nini kitatokea.
Mara baada ya tarehe 25 Oktoba tutakuwa na...
Zinaitwa Kampeni, na katika Kampeni za Kisiasa kuna njia kuu nne za kuwafikia wapiga kura ambazo ni;
1. Kukutana na wapiga kura moja kwa moja yaani Direct Voters Contact (DVC) kupitia Mikutano ya hadhara (Impact ni Ndogo kwa maana ya kuwafikia wapiga kura wachache)
2. Vipeperushi na machapisho...
Ana hulka ya ukimya na kutopenda kupayuka payuka kama ilivyo kawaida ya Wanasiasa wengi hapa nchini mf Mzee wa Mihogo. Anajua nini cha kuzungumza kwa wakati muafaka. Kama angeamua kujibu kila linalosemwa juu yake nadhani dakika 1440 zilizopo ndani ya siku angezitumia kujibu shutuma dhidi yake...
Lowassa anasifika kusimamia anachokiamini. Mimi sina shaka hata kidogo kwamba chini ya uongozi wake tutashuhudia TANZANIA MPYA tuitakayo. Anajua shida ya nchi hii. KURA yangu kwa LOWASSA, na wale wote wenye mapenzi mema tufanye hivyo na zaidi sana tumtafutie kura kwa watu wengine. Achaneni na...
Kama wamelaaniwa vile. hali ni hivyo hivyo TBC na StarTel. Yaani imebidi nizime tu Luninga. Aibu kabisa. Ovyo sana. Hata wafanye hujuma hizo sisi tumeamua wapi tunapeleka kura zetu. Sina wendawazimu kuipigia kura ccm wakti tunashindwa kufanya uzalishaji mali kisa UMEME unaletwa saa sita usiku na...
JFK.........Ni mtazamo wako tu ndugu, lakini ukweli ni kuwa nchi hii ilipofikia inahitaji Regeneration kuvua gamba. gamba ni watawala wa miaka mingi ambao ni hao ccm. U can not push a car when you are inside it. Newton's First Law of Motion proves this. Lowassa anatosha sana kufanya haya...
Mchakato wa kumpata Mgombea wa Urais kupitia UKAWA haukuja ghafla kama mvua ya Kiangazi. Mchakato ulikuwa mrefu na kujumuisha wadau wote chini ya UKAWA. Kama alivyokiri yeye binafsi kuwa alishiriki katika hatua za awali za kumkaribisha Lowassa ndani ya CDM na UKAWA kwa ujumla, iweje leo hii...
Kama CC itapitisha jina la Lowasa tutahitaji watusaidie kutoa majibu ya mswali haya;
1. Ile dhana ya kujivua Gamba ilimlenga Rost-m na nani? Tuliambiwa wapo watatu, wa pili ni nyoka wa makkengeeeza;
2. Fedha anayotumia kujitangaza kupitia vyombo vya habari na njia nyinginezo atazirudishaje?
3...
Na mtachapana sana mwaka huu. Ila huyo wa Matumaini haendi popote. Eti foleni Dar kwa miezi sita kwisha. Wapi na wapi? Huyu si ndio aliagiza njia tatu kipindi kile watu wakawa wanagongwa kila kukicha? Atakatwa tu. Mkateni Tu. Akatwe tu.
Hatimaye siku za CCM na Mulugo katika Jimbo la Songwe zinazidi kuhesabika mara baada ya Mwl. Frank Mwakitalima kutangaza nia ya kugombea Ubunge katika Jimbo la Songwe Mkoani Mbeya ambalo linaongozwa na Mhe. Philipo Mulugo. Kazi ya kutangaza nia ilifanyika kijijini kwao Saza na kuhudhuliwa na...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.