Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 59,042
- 132,825
Wanabodi
Jana nilibahatika kufuatilia mkutano wa Rais Magufuli uliofuta kikokotoo kipya na kurejesha cha zamani.
Taarifa ya Waziri Mhagama ilieleza uamuzi wa kikokotoo kipya ni kufuatia actuarial valuation ya afya ya mifuko iliyobaini mifuko ina hali mbaya ambapo kikokotoo cha 1:580
bado ni kile kile kwa sheria zote mbili ila tofauti ni malipo ya mkupuo kuendelea kulipa 50% kungeiua mifuko ya PSPS na LAPF hivyo ikaamuliwa malipo ya mkupuo yawe 25% kama ilivyo kwa PPF na NSSF ambayo malipo yao ya mkupuo ni 25% na sio 50% halafu ile 75% iwe distributed evenly for the rest of your life ambapo monthly pension inakuwa kubwa zaidi
Kiukweli kabisa nikisema sisi Watanzania ni watu wa ajabu sana au sijui niite ni ujinga tuu, kuwahi kutokea duniani, wanashangilia kikokotoo kile kile na hakuna tofauti ya formula ya kikokotoo bado ni ile ile!. Irene Isaka ametangaza mbele ya rais jinsi kikokotoo kipya kitakavyo wafaidisha wastaafu in a long run, hiyo 50% ni hela nyingi but short lived!, hebu someni bandiko hili mshuhudie jinsi tulivyo wajinga
Kikokotoo cha mafao ya pensheni kilirekebishwa Julai 2014, na ndicho kinachotumika hadi sasa, japo jina la kanuni limebadilishwa.
Kikotoo cha pensheni cha mwaka 2014 (hapo juu) kilinganishe na kile cha mwaka 2018 (hapa chini)
Hivyo wajemeni, kikotoo bado ni kile kile cha 1:580
Swali langu ni bila kuingilia mamlaka ya rais ku hire and fire as he pleases, kama taarifa hiyo ya actuarial ni kweli, mifuko ina hali mbaya, kosa la Irene Isaka ni lipi hadi kupelekea kutumbuliwa?.
Hii ni kufuatia kila anayetumbuliwa kuonekana ni jipu mbele ya jamii, kuna uwezekano baadhi wanaotumbuliwa sio majipu bali ni kondoo tuu wa kafara?.
Wataam wa masuala ya pensheni tufafanulieni, kama taarifa ya Waziri Mhagama imesema hali ya mifuko ni mbaya, kikokotoo kingeendelea mifuko ingekufa, sasa rais amekirudisha, jee mifuko hiyo italipa pensheni hizo nene kwa uwezo upi, tusije kujikuta kwa sasa tunashangilia tuu halafu baadae tunakuja kukaza mikanda kwa government bail out kwa hazina yetu?.
Utumbuaji: Tuache Siasa Kwenye Professionalism, Sio Kila Mtumbuliwa ni Jipu!. - JamiiForums
Utumbuaji Majipu wa Rais Magufuli: Is It A Right Thing, At The Right Time, And Doing It Right, Or ?! - JamiiForums
Hii Tumbua Tumbua ya Rais Magufuli, Hivi Kikwete Anajisikiaje?!. Anajisikia Sifa Au Anajuta?!. - JamiiForums
.
Jambo jingine la ajabu kuhusu pension ni ubaguzi wa wastaafu.
Jambo kubwa na la ajabu ambalo mimi kwa maoni yangu ninaona sio haki na sio fair, ni ubaguzi mkubwa wa mafao ya kustaafu kati ya viongozi wakuu na watumishi wa kawaida.
Mafao ya viongozi wakuu yanatawaliwa na Sheria ya Mafao ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1999, ambayo ilirekebishwa mwaka 2005, ambapo viongozi wastaafu wanalipwa pension kwa asilimia 80% ya mishahara ya walio madarakani, wakati wastaafu wengine wanalipwa mafao fixed kwa mujibu wa kikokotoo cha mfuko wa pesheni hisika.
Hii inawafanya viongozi wakuu kufaidika na kuongezeka pensheni mwaka hadi mwaka, wakati pensheni ya wastaafu wengine ni fixed!.
Wazazi wangu wote wawili, baba na mama ni wastaafu wa serikali. Baba tayari ni RIP lakini mama yupo na alistaafu mwaka 1990 akiwa ofisa wa juu wa serikali. Pension anayolipwa toka mwaka huo 1990 mpaka sasa is fixed, ukikisikia kiwango anachopokea, kiukweli, it's like a joke!.
Kwanini pension za viongozi wakubwa ziwe paged kwa percentage 80%, ya waliopo, lakini pension za wengine ni fixed kwenye kikokotoo cha mfuko ya pensheni?. Huu ni ubaguzi mbaya kabisa na sio kuwatendea haki wastaafu hawa!.
Utakuta mtu wa cheo cha Jenerali aliyestaafu 1990, analipwa pension ndogo kuliko Coplo au Sajent aliyestaafu 2015!. Is this fair?!.
And by the Way,
Ukimwangalia the way this lady look like, she looks like yule mama wa TIC aliyetumbuliwa, usikute...
it was just the most opportune moment to strike baada ya...
Kuna mambo mengine wajemeni yataka uwe na moyo haswa, sio mchezo...
hata ningekuwa mimi...
P