MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,255
- 8,027
Naomba kujuzwa kwanini tunapigia chapuo suala la mapinduzi ya viwanda nchini hasa awamu hii ya tano? Tulishafanya research kujua kuna demand ya nini hasa ili tuwe na viwanda vyake nchini badala ya kufuata bidhaa nje ya nchi? Isije ikawa ni kutekeleza Ilani tu bila kua na mpanga madhubuti.
Mapinduzi ya viwanda kule Ulaya yalianza tangu karne kadhaa huko nyuma kwa sababu wenzetu walikua kwenye tafiti za masoko hasa huku kwetu Afrika, waliona tunahitaji bidhaa kadhaa wa kadha na wakaanzisha mapinduzi ya viwanda ili kuzileta bidhaa zao kwetu Afrika na baadhi ya mataifa mengine yaliyokua yana demand kubwa kwenye bidhaa mbali mbali.
Sasa Huyu ndugu anayesema hata vyerehani navyo ni viwanda, ni sawa lakini hii inaweza kutupeleka kwenye mapinduzi ya viwanda? Kwa mawazo ya Waziri wangu huyu ni kweli tutasonga?
Mapinduzi ya viwanda ni suala mtambuka, demand haiko eneo moja bali ni kila sehemu inayogusa maisha ya kila Mwananchi. Tusikimbilie fulfilment ya manifesto ya chama bali kwende kwenye utafiti kwanza kama wazungu walifanyanini miaka ya 1800 huko.
Mapinduzi ya viwanda kule Ulaya yalianza tangu karne kadhaa huko nyuma kwa sababu wenzetu walikua kwenye tafiti za masoko hasa huku kwetu Afrika, waliona tunahitaji bidhaa kadhaa wa kadha na wakaanzisha mapinduzi ya viwanda ili kuzileta bidhaa zao kwetu Afrika na baadhi ya mataifa mengine yaliyokua yana demand kubwa kwenye bidhaa mbali mbali.
Sasa Huyu ndugu anayesema hata vyerehani navyo ni viwanda, ni sawa lakini hii inaweza kutupeleka kwenye mapinduzi ya viwanda? Kwa mawazo ya Waziri wangu huyu ni kweli tutasonga?
Mapinduzi ya viwanda ni suala mtambuka, demand haiko eneo moja bali ni kila sehemu inayogusa maisha ya kila Mwananchi. Tusikimbilie fulfilment ya manifesto ya chama bali kwende kwenye utafiti kwanza kama wazungu walifanyanini miaka ya 1800 huko.