Fuatilia kwenye u-tube kuna mahojiano kwenye mtandao wa sauti ya watanzania amemtaja kwa jina ally kibao kuwa anaongoza kikundi cha hamasa cha chadema wakati anajibu maswali ya Wana sauti ya watanzania
Tuachie mamlaka yatabainisha ukweli. Alisikika kwenye maswali aliyokuwa akijibu kwenye mtandao wa sauti ya watanzania akimtaja ally kama kiongozi hatari wa kikundi cha hamasa cha chadema na siku chache baadae mzee ally kauwawa kikatili.
Katika wizara ambazo zinakaba nchi kwenda mbele ni pamoja na hii ya TAMISEMI. Wizara hii ndiyo imekamata majukumu makuu ya kiuchumi kuanzia chini kabisa ngazi ya wananchi wazalishaji vijijini, miji midogo, miji ya wilaya, hadi miji ya mikoa. Ni wizara nyeti sana kwa maendeleo na ustawi wa...
Kama hayo yote yalitimia kutokana na sauti ya wengi, likiwamo la Yesu kusulubiwa, basi ni sauti ya Mungu kwa kuwa huo ulikuwa ni utaratibu wake wa kutimiza unabii. Bila hivyo unabii ungetimiaje?
Kwa kweli JK anatakiwa aseme neno moja tu kwa ajili ya kuliponya Taifa.
Mimi naamini, kwa heshima yake kama Rais mstaafu atasikilizwa na serikali pamoja na wananchi. Atoke hadharani, atumie hekima yake kuweka sawa suala la udini liloibuka. Wakristo na waislam sote ni wamoja tujirekabisha...
Hisia potofu tu hizi. Je nitakosea nikisema waislam wamejaa udini zaidi kiasi kwamba hawajadili vipengele vya mkataba badala yake wanautetea kwa sababu mwekezaji ni mwarabu mwenye uislam wake?
Acha kupotosha mkuu. Hayo unayoongea yote ni ya kihisia tu. Tusiharibu upendo wetu wa dini zote uliojengwa na watu wenye hekima zao. Hadi tuna baraza la amani ambalo linafanyakazi nzuri mno ya kuondoa ubaguzi wa dini. Huu uzi unachochea ubaguzi haufai kuendelea.
Mimi nashangaa sana. Hivi akili yetu yoote kuhusu uendelezaji bandari zetu ndiyo imeishia kwa DPW? Yaani hatuwezi kufikiri tofauti kabisa. Kwamba tukiachana nayo ndiyo tutakwama kabisa kuziendeleza wenyewe? Kwamba tumejidharau kiasi hicho. Yani ni sawa na baba wa familia mwenye mali nyingi...
Udini, udini na udini. Chuki, chuki na chuki. Hapa ni hekima, hekima na hekima inahitajika. Kumbe DPW ni bomu la udini. Hivi tukiachana nalo tutakifa? Maana tukiendelea nalo tutakuwa sikio la kufa halisikii dawa. Haya endeleeni na lugha zenu za kibaguzi. Msijesema hatujawambia siye kina voice of...
Ni kweli kabisa, kwa hapa tulipofikia kinachohitajika ni hekima ya Mungu tu ndiyo italinusuru Taifa. Mungu akautoe upofu wa uvyama, udini na utanganyika vs uzanzibari. Ukizuum vizuri huko mbele Taifa linaelekea kupasuka vipande vipande unless roho wa Mungu awashukie wazee wanaoheshimika na...
Kweli kazi tunayo watanzania. Kwa mwenendo wa mjadala kwenye Uzi huu unavyoendelea ni dhahiri vimelea vya udini vipo kwa baadhi ya watanzania.
Nafikiri ni bora tungejadili hoja zilizotolewa na wanaopinga mkataba huu kuliko kukazania tu kwamba wanaopinga wanapinga kwa sababu ni wakristo...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.