Haya tumeyasema mpaka koo zinakauka. Tunakoelekea siko kabisa. Naihofia sana nchi yetu hii. Elimu yenyewe ndiyo imevurugwa mpaka basi. Mungu atusaidie.
Ndugu yangu ukifuatilia mengi yanayoandikwa hapa unashindwa kuwaelewa ndugu zetu wengine. Hii jamvi ya JF yenyewe inaenda kufungwa mda si mrefu ila mtu yupo hapa kutetea kauli hizi za kudhibiti mitandao. Nafikiri tuna tatizo kubwa sana la elimu.
Hii ni kweli kabisa. CCM walidhani wanamzuia Mamvi lakini imekula hata kwao. Sasa kuondoka kutoka kwa hali hii ni kitendawili. Pili Tayari madhara ya hii miaka 2 (kama akibadilika au kuachia uongozi) makubwa sana tutayahisi muda mrefu.
Hamna haja ya kupoteza mda kujadili chochote na hawa watu. Ukisoma comment zao mbili tatu inaonesha kabisa fikra za kutopenda maoni badala. Wanaamini wakifungia watu wasiongee cha kupinga watazuia hata mawazo!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.