Recent content by rev

  1. R

    Hamadi Rashidi achoma moto misumeno 40 huko Visiwani Pemba

    Uchomaji wa Chainsaw unahusianaje na wapinzani jamani? Na hasa Mbowe anatoka wapi katika hili?
  2. R

    Vyombo vya Habari vya Ulaya vyazidi kuiandama Serikali ya Tanzania

    Mada tunayoizungumzia ni nyeti na haihitaji ushabiki wa kisiasa. Katika suala hili tusizunguke kama paka anavyouzunguka ugali wa moto. Ukweli ni kwamba, katika suala la Zanzibar, tumeikosea demokrasia na kuonyesha ubabe katika maamuzi. Hakuna kitu ambacho hakifahamiki nje ya nchi yetu...
  3. R

    Kusitishwa Msaada wa Marekani Uwe Mwanzo wa Kusitishwa Mingine

    Ninaomba nijitose kuzungumzia angalao kwa kifupi suala zima la Wamarekani kutunyima msaada. Mambo mawili yametuponza. Sheria ya kubana uhuru wa habari na uchaguzi uliorudiwa Zanzibar. Sheria ya kubana uhuru wa habari ni mbaya ambayo huko mbele hata wale waliounga mkono kupitishwa kwa sheria hii...
  4. R

    Tetesi: Siri ya Matokeo ya Uchaguzi wa Marejeo Zanzibar yaja juu

    Japokuwa inadhaniwa kuwa siri hiyo haijulikani, mioyo yao inawasuta sana. Yaani ni kwamba, watu wamemkataa Shein. Watu wameikataa serikali ya CCM. Sasa nchi itatawalikaje? Mioyo ya watu haimo na kiongozi wao. Hayo yatakuwa ndio matatizo ya ndani ya Zanzibar. Lakini kuna matatizo mengi zaidi nje...
  5. R

    Bomba la Mafuta: Kenya wamkomalia Museveni

    Hapa tunahitaji kuwa makini sana. Ukweli ni kwamba, as far as I know, Kenya are more smart in business than Tanzania and for sure they know how to manipulate. Sisi tulikuwa a bit hesitant and slow. Lakini mimi ninampongeza sana Raisi wetu. Alipokutana tu na Museveni hakupoteza nafasi. aliutumia...
  6. R

    TAMKO: CUF yatangaza kutoyatambua matokeo na hakimtambui Dkt. Shein

    Japokuwa sina upande wowote ninaoegemea, ukweli ni kwamba CCM na serikali yake wamefanya kosa baya sana. Haki imepokonywa waziwazi na kiubabe. Haki imepokonywa na bila haki pia amani haiwezi kuwepo.
  7. R

    Viongozi wa CHADEMA Arusha warudisha kadi

    Umaarufu wa Zitto ulimpatia jimbo moja katika uchaguzi uliopita. Uzembe wa Chadema wa kumwondoa Zitto umewapa majimbo mangapi?
  8. R

    Katiba Mpya: Askofu Kakobe ampelekea Rais Kikwete ujumbe wa wazi kutoka kwa Mungu

    Ujumbe huu wa Askofu Kakobe si wa kupuuza. Barua yake kwa Raisi Kikwete ni ya terehe 10 Machi 2014. Lakini yanayotokea sasa huko CCM yamepatana kabisa na unabii wa Kakobe. Hapa kuna ujumbe kutoka kwa Mungu hivyo tusiweke ushabiki wa vyama wala wa madhehebu ya kidini.
Back
Top Bottom