Ni bahati mbaya sana kwamba sisi tumekuwa na tunaendelea kuwa taifa la chawa (left, center and right). Ukitaka kujua ukubwa wa hili tatizo, angalia kule upinzani hali ikoje. Mwanachama wa CHADEMA, kwa mfano, akidiriki kumpinga Ayatollah Mbowe, BAVICHA na BAWACHA, bila kupoteza muda, wanamzika...
Fikra zingine hazina hadhi ya kuitwa fikra. Unaingizaje mtu Bungeni kwa mtutu wa bunduki ili ukamlipe mamilioni ambayo watu wengi wako tayari kuua wenzao kwa ajili yake?
Kuna watu wameshikiwa akili na watu wengine. Hawajui kwamba kuna political assassins ambao hawatumwi na mtu yeyote. Kwa mfano, yule chizi aliyevamia nyumbani kwa Nancy Pelosi na kumjeruhi mume wake kwa nyundo alitumwa na nani? Hawa machizi wetu wa hapa wangekuambia alitumwa na Trump!
Tangu lini mtu mwenye njaa akaweza kuenenda kama msomi? Professors wenyewe wanaopewa hizi assignments na watawala wanaweka usomi wako mfukoni, sembuse hawa pimbi ambao hata shahada ya kwanza hawajapata!
Kitu kinachofanyika kwa idhini ya mahakama hakiwezi kuhojiwa na kubatilishwa nje ya mahamaka.
Nionavyo mimi, hili ni swala la kifedha (fedha ya umma) ambalo linaangukia kwenye himaya ya CAG. Tukitaka kila mmoja wetu awe CAG hapa, nchi itakwenda ubenibeni!
Wana mfumo wa ajabu. Kila chuo kinapaswa kuwa na law school yake. Na jukumu la law school sio kumuandaa mtu kufaulu mtihani wa uwakili. Bar exam has nothing to do with law school. Sio kila law student anataka kufanya bar exam!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.