Nadhani atakuwa huko kwa siku kumi kwahiyo afya yake lazima itaimarika bhana.. Na nyie si mkapange foleni mpewe 'Parasetamo' halafu dawa zingine muandikiwe mkanunue ' Famasi yetu' mbona mnajifanya kufuatilia sana.. Alaah
Utafiti wangu aina ya 'quantitative research' baada ya kusoma uzi huu nimegundua umeandikwa na mtu mwenye uoga wa ghafla, njaa kali pamoja na ugonjwa wa Upungufu wa Akili Kichwani (UAKI)
Kama una kumbukumbu vizuri ndugu, suala la kubadilisha katiba lilipata nguvu mara baada ya Dr. Slaa alipotangaza kuwa moja ya mambo atakayoyatekeleza endapo angeingia ikulu..hivyo hilo linathibitisha hakuna anayehitaji katiba ya zamani..lakini mchakato ulioanzishwa na Mh. JK umepelekwa kichama...
Mkuu nahisi hujanielewa vizuri..maana yangu sio kuwa UKAWA peke yao ndo wana akili.. Maana yangu ni kuwa hii katiba hata uwe mwana CCM kindakindaki endapo utasoma vizuri bila kuweka uitikadi wa kichama, katiba hii ina mapungufu makubwa sana ukiacha hata hilo la serikali tatu. Mambo kama madaraka...
Maoni yangu ni kuwa uratibiwe mpango maalum na JF wa kuwapima akili wanaojiunga na mtandao huu ili kupunguza wimbi la mrundikano wa nyuzi zisizokuwa na ulazima wa kupotezeana muda kuusoma
Ahsante nngu007 kwa taarifa zaid..yaan hii serikali inayojiita sikivu ingekuwa inasikia kilio cha wananchi juu ya ufisadi tusingefika hapa tulipo.. Hapo tutakaoumia ni sisi wananchi kwa kucheleweshewa mishahara na sio wao
Kutoka katika ripoti ya Deutsche Welle (DW) leo mchana taarifa zinaeleza kuwa nchi wahisani wa Tanzania wamechelewesha misaada ya bajeti ya nchi ambayo ndio inasimamia shughuli kuu za taifa. Nchi hizo wahisani zijumuisha Norway, Sweden, Denmark, Uingereza, Finland, Ujerumani, Canada, Japan...
Hapo zamani za Kale palitokea mtu mmoja aliyekuwa na mengi ya kusema kama samaki lakini mdomo ulikuwa umejaa maji.. Alikuwa hana nauli ya kumfikisha mjini kwa 'Mjomba' kumueleza yanayotusibu. Mungu si Athumani alipata nauli lakini pia viatu kwa kuwa alikuwa akitembea peku.. Bahati mbaya sana...
Kama una akili timamu ungejiuliza kwanini ni haki kikatiba kuandamana..au kuandamana mnavyotafsiri nyinyi ni kuvaa mashati ya kijani na kwenda kumpokea kiongozi wa CCM basi??? Sikia ndugu yangu...watu wanapoandamana haimaanishi wanataka kufa kwa nguvu bali wanafikisha ujumbe kuwa hatutaki hicho...
Kweli umethibitisha Lumumba at work.. Yaani mmeshazoea mkiandamana mnafungwa skafu na mashati yenu mnafanana kama migomba inayotembea..hela yenyewe buku 7 siku nzima halafu mheshimiwa anaingiza siku na laki zake kadhaa.. Walahi bado tuko gizani na bila nyie tutafanikiwa tu
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.