Afadhali wewe ulihamia king'amuzi cha DSTv. Mimi ndio kabisa sina continenal, Dig Tek au hiyo DSTv na uchumi ndio huu wa mtanzania je tutamudu kuanza kutafuta ving'amuzi vingine?
Kama kweli unaipenda Tanzania na wananchi wake Ungeshauri vingine kwani tulio wengi tunahitaji ukombozi wa kweli. CCM wanachofanya kwa sasa nikutaka kupumbaza watu akili kwa kuzua mambo na kutisha wale ambao wanakikosoa.Hivyo tunataka mabadiliko CCM wakae kando na wengine waongoze wakishindwa...
Hata mimi nilimshangaa yaani mtu mmoja ndio mwenyeujua nyendo zote za Rwakatale. Inawezekana jamaa alihusika kwa namna moja au nyingine. Ipo siku kila kitu kitakuwa hadharani.Mungu ni mwaminifu.
Mungu ni mwaminifu siku zote. Cha msingi ni kusubiri kwani mbivu na mbichi zitaonekana. ukweli utawekwa wazi kweupeee kila mtu ataelewa ni upande upi unasema ukweli na upi unasema uongo.Maana yote yanayofanyika Mungu anayaona na siku ipo atayafunua kila mtu atashangaa.
Watu wa mkoa wa Kagera wanapitia kipindi kigumu sana.Matukio yaliyoonyeshwa na Kipindi cha ripoti maalumu ITV yanatisha na kusikitisha kwani watanzania wenzetu wanaishi maisha ya hofu kama wakimbizi. Naishauri serikali kuliangalia suala hili kwa jicho la tofauti na tupewe taarifa ya hatua...
Ni kweli hayo yanawezekana ila tunatakiwa watanzania wote tuamke kupiga vita vitendo vyote vya kifisadi ikiwa ni pamoja na viongozi kufanya nchi yetu ni mali yao na familia zao. Na tusipofanya hivyo 2015 tutabaki vilevile. Magamba nao wanataka kuhakikisha wanarudi kwa mbinu yoyote. Umoja wa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.