Mada ya msingi imetuelimisha kuhusu Hisa. Kinachofuata wadau ukisikia tangazo jiulize maswali yote au machache kwa kufuata mifano aliyotoa ili ujiridhishe kuinunua Hisa husika. Angalizo aliyotoa litufungue ili tuweze kuona mwisho kutokea mwanzo vinginevyo utajiingiza kwenye mlango usiohusika.
Mkuu somo hili zuri sana, lina kila jibu la maswali yanayohisiana na Hisa na kadhalika. Nikuombe ushauri kwa watu kama mimi tuliowahi kununua Hisa za NICOL ambayo hatimaye imefutwa ama kujifuta kwenye soko la Hisa. Matarajio kutokana na uhamasishaji uliofanywa ndani ya nchi na nje kwenye Balozi...
Mkuu, mara kadhaa nimesoma Mada kuhusu Hisa, na elimu ilitolewa ilinifikisha mahali pa kudhani kuwa nimepoteza. Kama yupo anayejua lolote kuhusu Kampuni hii anisaidie kwani nina Hisa zangu tangu miaka ya 2004/2005.
Inasikitisha kusikia huduma hasi kwenye Kampuni iliyobeba nembo ya TZ. Hawa ATCL tunaoambiwa wako mbioni wayaangalie maoni ya WATEJA wasafiri wa mara kwa mara kwani watakapoingia wateja ndio hawa hawa.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.