Wakuu Habari,
Tangu timu hizi mbili za Kariakoo kuvuka hatua ya nusu fainali, mengi sana yamejitokeza kwa baadhi ya mashabiki hadi viongozi wa serikali. Tunafahamu kweli faida ya kupeleka timu mbili robo fainali na wengi pia tunatamani ikiwezekana mmoja achukue kombe hili ambalo halijawahi...
Kwa mfano leo, wewe mwanachi wa Young African unayetamani mnyama afungwe, umekaa chini ukajitafakari kwa makini kwamba ni sahihi unachofanya? Wabongo tuko tayari kushabikia al hilal au mazembe ila sio vya nyumbani. Hujachelewa, anza sasa
Utani ubaki ligi kuu huku kwingine tupeane support
Kumbe unanifahamu mkuu, sema mi mweusi ila upara kama gamondi.
Cha msingi tubadilike, kila timu ipambane na malengo yake. Biashara ya wasemaji wa hizi club kuanzisha vijimaneno vyao hapa vya kutujaza chuki visitufanye tusiwe wazalendo kwa kuipenda nchi yetu.
Mkuu hata kama una jirani yako na humkubali kabisa, akipata changamoto huwezi kushangilia hadharani kama inavyotokea hapa Tanzania. Na huu ujinga naamini umekolea zaidi hapa Tanzania na ukichochewa zaidi sana sana na wasemaji.
Hapa sipo upande wowote mkuu, nashangaa tu inakuaje hapa bongo unakuta kuna mashabiki wa medeama? Au wa wydad? Ina maana hatupendi nchi yetu iwe na mafanikio kwenye mpira? Watakuja al hilal na tp mazembe watapata mashabiki wa kutosha kwa mkapa ila kwa sisi wabongo dah support kwa timu ikiwa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.