Kazi yoyote ya kuajiriwa ni utumwa mkuu
Kama nilikuwa Tanzania na sikupata kazi ya kujipatia angalau pesa ya kula,ila nimekuja huku nina uhakika wa kupata pesa kila mwisho wa mwezi na nikapata angalau chochote cha kutuma nyumbani basi ni bora niendelee kuwa mtumwa
Hizi story za humu ndio ambazo zinawafanya watanzania wengi mpaka sasa waogope hata kutoka kwenda nchi ya karibu kwenda kufanya kazi
Kuna sehemu unafika na ukasema ww umetokea Tanzania wanaanza kukushangaa,kwasababu wanajua sisi ni waoga sana wa maisha nje ya nchi yetu
Sheria za kazi zipo...
Nakuelewa mkuu hata mimi nilikuwa na mentality kama yako ila maisha yaligeuka na nikawa sina namna,nikaja huku nikapambana na leo hii nashukuru kwa hatua niliyopiga
Nikwambie tu ukweli wa hapa hasa UAE
Vyeti vya nyumbani kwenu havina msaada wowote,ukifika kwa mara ya kwanza kubali kufanya kazi...
Yeah ni sahihi kabisa na ndio maana kwenye kazi hizo wamejaa Wa bangladesh,na wanepal kwa africa wamejaa Uganda na Burundi ila kwasasa ndo nimeanza kuona watanzania wapo wanajipambania kwenye kazi hizo
Hapana kaka mimi nimeishi Dubai kwa mshahara huo na nikikuwa nafanya saving ya laki 4 kwa mwezi
Kwa maana ya kwamba nakula laki 2 na natuma nyumbani laki 1 halafu iliyobaki nasave
Kwasababu malazi,usafiri na matibabu ni bure na hvyo ndo vitu ambayo vina gharama sana
Dubai sio sehemu ya kuja...
Mtu ambaye atakufanyia utaratibu wote huko Tanzania ni mwajiriwa wa serikali hiyo dhamana tosha pia unaweza kuja na mwanasheria wako kwamba unatoa pesa yako kwa ajili ya safari na ikienda tofauti utahitaji kurudishiwa pesa yako na mikataba ikasainiwa
Ni sahihi kabisa mkuu,hizi mentality ndo ambazo zinatufanya watanzania wengi kudumaa kwenye ufikiri
Tunasahau pia kwenye growth of careers na kupata new opportunities,Dubai ni ardhi ya opportunities
Naweza kujitolea mfano mm nwenyewe nilipoingia Dubai miaka 3 iliyopita kwa mshahara wa 900...
Bongo mshahara wa laki 7 anaupata mwalimu,ila ukiwa mgaigai wa kufanya kazi kwenye sekta binafsi tena unskilled labour huwezi kupata hata mshahara wa laki 4 kwa mwezi
Kiongozi naona unapiga hesabu za rent za kuishi kwenye apartments ila sehemu za kuishi au kulala hapa UAE zimegawanyika kama ifuatavyo,kuna Bed space ambayo kwa mwezi inaanzia 200aed hadi 1000aed,pia kuna partition hizi zinaanzia 1000aed hadi 2000aed pia kuna chumba kizima hapa unalipa kuanzia...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.