Mkuu uajua kwanini huko nyuma mtoto wa mlamba asali alikuwa na nguvu sana, jibu ni kuwa yeye na swahiba wako mandondo ndio walishikilia code za mfumo wote, hii ikawa inampa kiburi mbele ya wamiliki wa shamba la mboga mboga, walichokifanya ndicho hicho unachokisema, kifupi wakaanza upya nje ya...
Mkuu hakuna kitu cha independent observer kuangalia mfumo, haya mambo ndio hata tume kule Kenya huyafanya, pamoja na mahakama kuiambia tume ifungue server hadi leo tume haijafanya hivyo. Kuna uhuni mwingi kwenye hizi chaguzi na si Africa tu hata Marekani pia nadhani umemsikia Trump akilalamika...
Pamoja na kutokuwa muumini wa Lissu leo nimeumia sana kwa haya yanayoendelea kuhusu Lissu, nimepata uchungu wa mzazi kwa mwana, sijui Lissu kawakosea nini kwa haya yanayoendelea, roho zitawasuta hadi makaburini.
Acha upumbavu mkuu, wenzetu ili uwe raisi unatakiwe uwe na akili timamu na afya njema, sasa huyu Mzee hali aliyonayo hata kumukumbuka mwanawe hawezi unataka ndie agombee uraisi hata Biden aliambiwa aondoke kutokana na changamoto ya kiafya sembuse huyu Mzee.Cheyo, kwa hiyo hali kweli atazunguka...
Mkuu huyu hana tofauti na brig Moses Ali wa Uganda ni vituko lakini najiuliza huyu mzee mapesa hana watoto au mke wa kumshauri kuwa sasa mzee huku ni kudhalilisha jina la Cheyo, hizi ni njaa gani jamani mbona watu wanaishi tu bila ya kuwa wanasiasa? hii ni aibu na fedheha kwake na wanafamilia...
Musukuma mnafiki sana, huyu alikuwa kundi la Lowasa na hata kwenye kampeni pale uwanja wa Sheikh Amri Abeid alishuka na helicopter pia akiwemo Juma Awesu, Kingunge Ngombale Mwiru, Nchimbi, Anna Tibaijuka.
Mkuu nimeskitika wazee wazima wameufyata japo mzee Butiku nae amejifanya kuongea lakini kawa muoga anazunguka mbuyu, labda mzee anaogopa kuambiwa na wewe una mawaa kwenye Kigoda cha Mwalimu.
Na tayari aliaga kuwa ikifika 2025 hatagombea tena, wacha yampate kama yaliyompata Mzee wetu kule kwa Kibajaji hadi ikawa aibu kwake aliposhindwa na mhuni Kibajaji.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.