Wananchi wapo? Wanatoka wapi na wametangaziwa wakishapiga kura waende nyumbani?
Hembu nikuulize, kwa hiyo unadhani hizo kura fake ziko kwa ajili gani? Za maonyesho au? Kwamba wahusika wawe na kura feki halafu wasijue wataziingizaje?
Unawezaje kutuuliza sisi wakati wenye kura feki ndio wanajua...
Umenena vyema, ila usingizi walionao wangeamka wote kwa pamoja nyakati hizi wangeupata ukombozi wao wenyewe.
Hiki ndio kipindi waandishi wana umuhimu kuliko kipindi chochote kile lakini wameshindwa kukitumia.
Yaliyomkuta Kabendera yalipaswa kutolewa majibu kipindi hiki kuliko wakati mwingine...
Bila kusahau Kifo cha mama yake na Mwandishi aluyebambikiwa Kesi na mpaka kufikia kumuomba Raisi amuachie mwanaye huru.
Ni ajabu waandishi bado hawaoni kuwa hawako Huru
Huyu mtoto wa dada alipata kesi ya mauaji Kanisani, haijapita mwaka Dotto naye kapata kuhusika katika chain ya maswali tata juu ya kifo cha Lwajabe, hii familia inatatizo gani na damu za watu
Wapwa wametamalaki Kipindi hiki cha miaka mitano, hivi niulize ni huko tu mjini ndio watoto wa dada zetu wanavimba au hii familia ya huyu bwana?
Hivi hana mtoto wa kiume angalau angewacontrol watoto wa dada kama alivyofanya Riz wakati ule??
Hii Lissu aitumie vyema kufafanua umuhimu wa Uhuru wa wananchi kufanya mambo yao bila kuingiliwa na watawala.
Uhuru, Haki na Maendeleo sera bora kabisa katika zama hizi za utawala wa kidikteta
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.