Recent content by Lukonge

  1. Lukonge

    Hizi ni dawa hatari kwa figo zako

    Jambo moja mhimu la kufahamu, dawa yoyote ni SUMU inaweza kuleta madhara ndani ya viungo vya mwili. Kinachotofautisha hapo ni kuzingatia kiasi gani cha dawa unatakiwa kuchukua, kila baada ya muda gani na kwa urefu wa kipindi gani. Tusipofuata utaratibu hata maji ni sumu, Panadol ni sumu nk.
  2. Lukonge

    Naomba msaada wa afya naombeni msaada

    Pole kwa kuumwa. Mambo mhimu ya kuelewa na kuzingatia: 1: Rufaa au kuomba rufaa ni moja katika haki za msingi pale unapokuwa na sababu ya/za mhimu. 2: Kabla ya kuomba rufaa jitahidi kuwasiliana na mtoa huduma wako ili kujua tatizo lako la msingi, matarajio ya daktari kulingana na unavyoumwa na...
  3. Lukonge

    Maziwa ya mama kukata ghafla

    Stress homoni kama Cortisol husababisha mrejesho hasi/negative feedback kwa homoni zinazohusika na kuzalisha maziwa kama Prolactin na hivyo kuathiri kwa kikubwa kiasi cha maziwa yanayozalishwa.
  4. Lukonge

    Wafanyabiashara takribani 90% wana maisha magumu. Kijana usidanganyike na mafanikio ya wachache, Business is not for everyone!

    Wasilisho zuri 1: Unaonyesha kuwa na mawazo au uzoefu mzuri na kwa nia njema unashirikisha ili kuonyesha hali halisi ilivyo. Ingawa kunahitajika kuwa na data au rejea ya tafiti au andiko linalotambulika ili kuyapa uzito halisi mawazo haya kwa upande husika. 2: Kufanikiwa/kuvipita vihunzi hivi...
  5. Lukonge

    Kwanini siponi amoeba

    Pole kwa kuumwa. Kuna vitu vya kuzingatia: 1: Historia ya kuumwa kwako haijasadifu sana mgonjwa wa Amoeba kama ni kutibiwa kwa eneo ambalo mtaalamu wa afya hawezi kupata vipimo/symptomatic treatment. Mgonjwa wa amoeba hupata maumivu makali ya tumbo ya kukamua/kubana/cramping. Kwa siku za...
  6. Lukonge

    Chronic headache

    Haya ni.maelezo ya jinsi ya kutafuta suluhu ya maumivu husika, kwa mtu ambae maumivu ni makali kwa wakati husika: 1: Kuna vitengo vya dharula kama hauko vyema. 2: Pia, Nurse anaempokea mgonjwa kwenye maeneo ya OPD/wagonjw wa nje hutoa taarifa kwa daktari kulingana na hali ya mgonjwa ili kupewa...
  7. Lukonge

    Chronic headache

    Mambo mhimu ya kuzingatia: 1: Fika kituo cha afya/hospitali. 2: Onana na daktari ukiweza kumwona daktari bingwa wa magonjwa ya ndani/physician itakuwa vyema zaidi. 3: Utahitajika kutoa historia ya ugonjwa wako kikamilifu. Jinsi kichwa kinavyouma, ukali wa maumivu unaongeka kadri siku...
  8. Lukonge

    Swali la Kikatiba na Kisheria: Chadema wanataka Reforms kabla ya Uchaguzi Mkuu, pendekezo au takwa hili wamelifikisha mamlaka ipi ili lifanyiwe kazi?

    Huko unakowazia yapo mengi tu yamerundikana hayajatekelezwa. Kusikia kwa kenge........., kwani hii imetekelezwa? Au kupigishana raundi tu. Mwananchi Mahakama ya Afrika: Mgombea binafsi halali kushiriki uchaguzi...
  9. Lukonge

    Swali la Kikatiba na Kisheria: Chadema wanataka Reforms kabla ya Uchaguzi Mkuu, pendekezo au takwa hili wamelifikisha mamlaka ipi ili lifanyiwe kazi?

    Kama chama na wadau wa demokrasia: 1: Walishakaa vikao na Rais aliyepo madarakani akihusisha wahusika mhimu kwenye baraza la mawaziri, kwa nyakati tofauti kupitia yatokanayo na chaguzi zetu kuu mbili zilizopita na kuona wapi tulifanya vyema na wapi hatukufanya vyema pia uhitaji wa mabadiliko...
  10. Lukonge

    Naomba sababu ya Kiufundi na ya Kiutaalam kabisa kwanini huyu Nyoka HATARI hapa hakumuuma huyu Mtoto

    Wanasayansi wanaamini kuwa, nyoka huweza kunusa harufu ya kemikali ambazo mtu/au mnyama mwingine hutoa anapomwona nyoka kama mjongeo wa hatari(fight vs flight). Chekali hizo ni kama Cortisol na Adrenalini kwa uchache. Uwezo wa utoaji wa kemikali hizi hutokana na utambuzi wa hatari husika/nyoka...
  11. Lukonge

    GE2025 Samia Suluhu Hassan ni Mgombea Halali Kikatiba na kihistoria

    Mhula wa urais una miaka mingapi kikatiba? President by default unaita mhula, kwa katiba ipi imehesabu ni mhula wake wa kwanza. Sawa hata ukisema ni mhula: Amewaomba lini wana CCM kuwa anataka kuendelea/kuanza? 1: Unaenda kumkabidhi mtu nchi bila yeye kuomba na kuonyesha utayari, mwaka kesho...
  12. Lukonge

    Nani yupo nondo kati ya alie fanya Masters au aliesoma vitabu vingi kwenye eneo husika?

    Hapa suala kuu ni nondo/knowledge vs njia uwasilishaji mtu apokee na kutumia vyema. Tunapimaje nondo/knowledge asseasment? 1: Je tunafikiri kila mtihani unabeba uzito/mantiki sawa? Sikusema maarifa hayapimiki bali kupima kwa usawa ndo tatizo(topiki ipi, upime wapi, kwakiasi gani obejective na...
  13. Lukonge

    Nani yupo nondo kati ya alie fanya Masters au aliesoma vitabu vingi kwenye eneo husika?

    Hili swala ni gumu sana hasa tukienda kwenye msingi wa kuwa nondo kama uelewa/maarifa na uwasilishaji vs uwezeshi/knowledge. Ili kupima uelewa inabidi upime maeneo mengi kwani inahusisha: 1:Uwezo wa kurudia kitu husika 2: Uwezo wa kutafsiri kitu husika 3: Uwezo wa kutumia maarifa husika 4...
  14. Lukonge

    Nani yupo nondo kati ya alie fanya Masters au aliesoma vitabu vingi kwenye eneo husika?

    Suala kubwa ni ubebaji wa maarifa halisia yenye matokeo chanya kwenye jamii na namna ya upatikanaji wake ndo msingi mkuu.
  15. Lukonge

    Nani yupo nondo kati ya alie fanya Masters au aliesoma vitabu vingi kwenye eneo husika?

    Ndiyo. Je njia ya kupata maarifa inaweza kujisimamia kwa mtu huyo kuwa nondo?
Back
Top Bottom