Recent content by Lukonge

  1. Lukonge

    JamiiForums Tanzania Ni njia gani sahihi ya kujikinga na U.T.I wakati wa sex?

    Si kweli, tatizo liko kwenye kutanabaisha ulichokipata ni UTI au STI? Ukikutana kingono na mtu mwenye STI utapata STI. Ukikutana na mtu mwenye UTI hautaambukizwa UTI kwani hii si njia rasmi ya kuhamisha mdudu husika. Hivyo, ndo maana ukisoma jinsi ya kujikinga na UTI utaambiwa: 1: Kunywa maji...
  2. Lukonge

    JamiiForums Tanzania Ni njia gani sahihi ya kujikinga na U.T.I wakati wa sex?

    Jambo la kwanza naoma TUTAMBUE: 1: UTI: Urinary Tract Infection ( maambukizi ya njia ya mkojo). 2: STI: Sexual Transmited Infection(Maambukizi yatokanayo na tendo la ngono). Hivyo, UTI si STI Kwani wadudu wanaoambukizwa kwa njia ya ngono wamejitanabaisha/kuwa na uwezo wa kuambukizwa kwa njia...
  3. Lukonge

    JamiiForums Tanzania Siku hizi kuna mlio hua nausikia kupitia sikio la kushoto ambao wengine hawausikii

    Fika kituo cha afya ili kuangaliwa masikio. Hii inaweza kuhusisha: 1: Shida kwenye sikio husika (nta, matumizi ya sauti kubwa/kusikiliza, mshipa wa fahamu kwenye sikio husika au ngoma ya sikio). 2: Tatizo tokaceneo jingine la mwili kuathiri sikio ( matumizi ya dawa, ongezeko kubwa la presha au...
  4. Lukonge

    JamiiForums Tanzania Ni sahihi John Heche kumuacha Dereva wake kwenda kulala Chumba cha Sh. 3,000/=?

    Kwa hiyo madai ya J. Heche kuwa wa mwisho kuonekana na marehemu umeyaondoa. Sasa unatengeneza ya gesti ya 3,000/=!!?? Hivi kuna watanzania wangapi wanalala mazingira ya chini ya gesti ya 3,000/=!? Na ukizingatia wengine ni waajiriwa wa serikali, unataka kueleza nini hapo!? Tusipende kila...
  5. Lukonge

    JamiiForums Tanzania Kifo cha Dereva wa John Heche Polisi wamepata pa kuanzia, waanze na John Heche kufanya uchunguzi

    Wewe umejuaje alikuwa wa mwisho? Huoni kama wewe unaethibitish hili ndo ulikuwa shuhuda wa mwisho?
  6. Lukonge

    JamiiForums Tanzania TMDA yapiga marufuku dawa yenye kiambata cha levamisole

    Pamoja na kwamba sijaiona taarifa husika kwenye site ya TMDA, hili ni jambo la kawaida kwenye suala la Uvumbuzi na Uendelezaji wa dawa, vifaatiba na viambata duniani kote. Dawa inapokidhi vigezo na taratibu za kutumika kwa binadamu, huruhusiwa kwa kuendelea kufanyiwa kitu kinaitwa Post Market...
  7. Lukonge

    JamiiForums Tanzania Naomba ushauri kuhusu tatizo la Mke wangu la mfumo wa Mkojo lililodumu Miezi 7

    Pole kwa kuuguliwa. Kuna sababu nyingi zinazoweza kuleta tatizo hili kutokuisha: usugu wa dawa, mdudu kujichimbia kwenye ukuta wa kibofu, tatizo la misuli ya kibofu, mabadiliko ya homoni, tatizo la misuli ya sakafu ya nyonga na tatizo la mwingiliano wa matatizo ya njia ya uzazi. Hivyo, tatizo...
  8. Lukonge

    JamiiForums Tanzania Watoto wote wanne (4) siyo wa kwangu, wanawake mna roho ngumu

    Kuwa makini na ulichokitafuta: DNA haipimwi kirahisi/kwa utaratibu unaojulikana na kwa kipindi kifupi/ndani ya muda mfupi hivyo. Ulipeleka stori na umepewa majibu kulingana na stori yako. Ingia kwenye tovuti ya maabara ya mkemia mkuu wa serikali uuone utaratibu. Usijekuwa umepimwa blood grupu...
  9. Lukonge

    JamiiForums Tanzania Muungano wetu na methali ya mchelea mwana kulia, hulia mwenyewe

    Uhusiano wa kweli "usio na hoja kati ya wanaohusiana" ni kama hadithi tu au haupo na haujawahi kuwepo na hautakaa uwepo. Hii ni kwa sababu hakuna watu wawili wanaofikiri, kuhisi au kuitikia sawasawa. Tofauti au kutoelewana ni jambo lisiloepukika kwa watu wawili. Je kwa muungano wa nchi...
  10. Lukonge

    JamiiForums Tanzania The Voices From Within:Kilichotokea Oct. 29 Japo Anayeonekana ni Yeye Kumbe Si Yeye Kuna Watu Hawakutimiza Wajibu Wao Ndio Wamemponza, Tumsamehe Tuu?

    Paskali, Tatizo unataka kuwa potepote, mwisho wake unaandika na kujikanganya mwenyewe. Ukitaka kuelewa haya mambo, soma post namba sita (6). Kufahamu uhusika wa mhusika kwenye tukio, ni muhimu kutizama matendo yake: 1: Kabla ya tukio 2: Wakati wa tukio 3: Baada ya tukio Wewe ni mwanasheria...
  11. Lukonge

    JamiiForums Tanzania Uchawa ni mfumo, bila Katiba mpya hauwezi kuisha

    Daktari! Hongera kwa andiko. Binafsi nakubaliana nawe, lakini nina angalizo juu ya hili au mtizamo wa nyongeza. Katiba peke yake si suluhisho la kutoka hapa tulipo. Hapa tulipo tatizo bado si katiba peke yake bali tumekengeuka tangu kwenye malezi kuanzia ngazi ya jamii/familia. Naamini...
  12. Lukonge

    JamiiForums Tanzania PostGE2025 Kwa hapa tulipofika; Ya Oktoba 29 tungeyaacha, tuendelee na mambo mengine

    Daktari, Mambo haya huwa hayajifii/hayamalizwi kwa kusema tuyaache. Sayansi ya jamii inasema hatua muhimu kwenye kujenga mahusianao mema/reconcilliation: 1: Aliyekosa/akubali kutenda makosa kama yapo. 2: Onyesha kujutia kwa kilichotokea/kubali kubeba lawama na thamani ya tatizo husika. 3...
  13. Lukonge

    JamiiForums Tanzania Hizi ni dawa hatari kwa figo zako

    Jambo moja mhimu la kufahamu, dawa yoyote ni SUMU inaweza kuleta madhara ndani ya viungo vya mwili. Kinachotofautisha hapo ni kuzingatia kiasi gani cha dawa unatakiwa kuchukua, kila baada ya muda gani na kwa urefu wa kipindi gani. Tusipofuata utaratibu hata maji ni sumu, Panadol ni sumu nk.
  14. Lukonge

    JamiiForums Tanzania Naomba msaada wa afya naombeni msaada

    Pole kwa kuumwa. Mambo mhimu ya kuelewa na kuzingatia: 1: Rufaa au kuomba rufaa ni moja katika haki za msingi pale unapokuwa na sababu ya/za mhimu. 2: Kabla ya kuomba rufaa jitahidi kuwasiliana na mtoa huduma wako ili kujua tatizo lako la msingi, matarajio ya daktari kulingana na unavyoumwa na...
  15. Lukonge

    JamiiForums Tanzania Maziwa ya mama kukata ghafla

    Stress homoni kama Cortisol husababisha mrejesho hasi/negative feedback kwa homoni zinazohusika na kuzalisha maziwa kama Prolactin na hivyo kuathiri kwa kikubwa kiasi cha maziwa yanayozalishwa.
Back
Top Bottom