Mkuu Salary Slip naamini BoT wamekusikia. Najua kuna Mkurugenzi mpya wa Usimamizi wa Sekta ya Fedha, very active, hataacha hili lipite bila kulifanyia kazi kama kuna ukweli. Najua anatembeleaga humu.
Nakushauri ufikie Retaj Hotel. Bei ni kati ya USD 55 mpaka USD 80. Bargaining power itasaidia kupunguza. Usitegemee makubwa, ni pa kawaida sana na vitu vingi wanafungasha Kariakoo. Ukienda na ATC utaona Wakomoro wanavyofanya shopping Bongo. Kama unapenda maisha ya usiku ukifika wenyeji...
Mkuu Faana umetaja suala la kuwasaidia maskini, wajane, wagonjwa na mayatima. Hakika limenigusa sana hasa kuona ambavyo binadamu tumejisahau kuyasaidia haya makundi wakati tukionesha ufahari katika maisha na nyumba za ibada. Kuyasaidia haya makundi ni miongoni mwa ibada kubwa kabisa!
Lanlady nakubaliana na hoja yako ambayo ni ya msingi sana!
Mfano baada ya ripoti ya CAG watu tumejikita kubishana ni awamu ipi imesabibisha ufisadi uliotajwa badala ya kujumuisha nguvu pamoja na kuonesha hasira zetu juu ya huo ufisadi na madhara yake kiuchumi, kijamii na kwa maendeleo ya taifa...
Sawa ila haya yalitokea pia wakati wa Magufuli. Hii ripoti ni ya 2020/21. Ukweli ni kuwa upigaji Uhamiaji umekuwepo siku nyingi pamoja na kuwekewa mifumo ya ulipaji. Wafanyakazi kwy viwanja vya ndege ni kawaida kabisa kuwaambia wageni mfumo uko down hivyo wanalipa manually. Hapo unategemea nini...
I fully agree with you. Tatizo la vichaa wetu ni level ya ukichaa kufuata uchumiaji tumbo! We need leaders who are consistent and who would constantly be there for broad interest of the nation. Tusiwe watumwa wa matumbo yetu!
Ni kweli ana hoja ndo sababu nchi kama Marekani rais anakabidhiwa national policy ambayo inampa direction ya nchi. Shida yangu ni moja tuu, je Magufuli angekuwa hai Gwajima angeongea haya?
Kuna kundi lilidhani system haiko na mama, linakosea. Baada ya huyu muungwana kuongea 26 Dec siku iliyofuata mtu akapewa ki-note akaongee Clouds Power Breakfast, jana wametumwa zoom meeting, leo yeye mwenyewe kaambiwa aombe msamaha.
Mama zunguka uilete dunia Tanzania. Lazima tuende na utandawazi hatuwezi kujifungia. Tunahitaji wawekezaji. Zaidi ukitoka watasema, ukijifungia watasema!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.