Kwamba "FOREVER"?!? Tena inaandikwa kwa herufi kubwa!!
This is terrible!! Sasa Tundu Lisu aandae koromeo vizuri, kama huyu wanampa kifungo cha Kimya kimya
Yeye anazodolewa kwasababu amesaliti imani aliyowalisha hao aliowaleta na kuwatengeneza. Ni sawa na muhubiri anayekana mahubiri yake mwenyewe kwa vitendo lazima waumini wenye akili watamshangaa
Pesa huisha, mwanzo nilikuwa na fikra kama hizi ila baada ya kusoma kwa tafakuri maandishi yake; huyu bwana inaonekana hata hela zimemkimbia kwasababu ukiwa na hela dunia hii hukosi marafiki wenye hela pia
Wewe jifunze kwa kina Makongoro Nyerere, Madaraka Nyerere wanavyoishi maisha ya kawaida yasiyo na tamaa ya madaraka wala kujali kwamba Mzee wao aliwaongoza wazalendo wa wakati huo kupigania uhuru wa Taifa hili kwa ajili ya watanzania wote na si kulifanya Taifa kuwa mali ya familia
Ndugu Hamisi Kingwangwala ni somo tosha kwa wabunge wa ccm kwasababu aliwahi kuwa mbunge;
Ni darasa kwa mawaziri wa sasa kwasababu aliwahi kuwa waziri,
Ni elimu inayoishi kwa kila kiongozi wa serikali anayedhani nafasi aliyonayo ataishi nayo milele,
Ni fundisho kwa wote wanaodhani kwamba...
Niliwahi kusema mahali kwamba hata yule Charles wa wasafi ukimuweka na Odemba, Charles yuko vizuri zaidi kwenye kuuliza maswali kuliko Odemba
Kinachombeba Odemba ni ule "ung'ang'anizi" wake wa swali kwa mtu anaye hojiwa lakini bado anatakiwa kujinoa zaidi
Mambo yamebadilika sana kizazi hiki
Ukiwasikiliza wanajinasibu kuwa vijana ndio nguvu ya Taifa utafikiri hizo nguvu wanazo kweli
CCM imefanikiwa kwa kiwango kikubwa sana "kuwaua" vijana! Haijawaua kimwili lakini imewaua kifikra na kijasiri
Ukisoma historia ya wapigania uhuru wengi wa Afrika...
Nikiwa mdogo kama walivyo watu wengi kuna mambo unakuwa huyaelewi elewi na kadiri unavyokuwa ndivyo unavyoendelea kupata ufahamu
Nikiwa mdogo nadhani hadi umri wa kidato cha Pili (hapa sio mdogo tena hii ilikuwa imani) tungegombana endapo ungeniambia "nafaa" kuwa mwanajeshi au uniambie nikiwa...
Hata yule wanayemuita sijui Mjomba mwenye herufi baada ya "S" naye hujitetea sana kwa kulambalamba midomo hivi hivi kama unavyofanya wewe wanapomwambia ukweli. Sijasema wewe ni yeye ila ndege wanaofanana huongea lugha moja
Awamu hizi mbili hasa hii ya sasa imejua sana kudogosha vyeo vya viongozi wa serikali
Siku hizi hakuna mtu anatishika na kauli za waziri wa mambo ya ndani hata kama ni za amri kwasababu vyeo vyao wamevifanya kuwa vya mambo yasiyoeleweka. Hii inaondoa hadhi ya kiuongozi
Kwa mfano, hizi drama...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.