Mimi mwenyewe nina wasiwasi na huu mgao wa kinyemela.Nawashauri mawakala wa vyama pinzani kujiandaa na tochi za mchina in case lolote litatokea. Huu mpango utaendelea hadi siku ya kupiga kura wahusika amkeni!!
Wanabodi, huyu FaizaFoxy ni mmoja ni mmoja wa wachaingiaji ambaye michango yake ni ya kidini na uchochezi wa kikabila wa hali ya juu lakini mods wanamuangalia tu! naomba vyombo vya kufuatilia waharifu wa makosa ya kimtandao waanze na huyu. Wakishindwa nitaamini anatumiwa kimkakati.
Acha chuki binafsi. Kauli ya huyo Bulembo ni ya kichochezi tofauti na ya Lowassa.Kusema wapinzani hawataingia ikulu ni vitisho na uchochezi tume ya uchaguzi hatua kwa huyu mtu.
Mkuu Mag3 heshima kwako. Nimekuwa nikifuatilia thread zako hakika zimejaa weredi mkubwa na uchambuzi wa kina. Nikirudi katika mada husika, uliyoyasema ni kweli hakika. Tukumbuke wahenga walisema "ukiua kwa upanga utakufa kwa upanga".Hayati Bob Marley anatukumbusha "what comes around goes around"
Kati ya wanajamvi wadini na wakanda huyu the Big Show anawapiku wenzake humu kwa mbali sana. Tangu nimemfahamu humu yeye ni mada za udini, ukabila na ukanda basi! Wadau nadhani mnakumbuka wakati wa sakata la mafuta na gesi Lindi na Mtwara ni huyu huyu The Big Show aliyekuwa anakuja humo...
Juliana, ingekuwa na busara iwapo ungeleta uzi ukiwa na hizo video za hotuba za Nape na Kinana ili tuchague mchele kati ya chuya. Ulikuwa unawahi nini?! Kuna mashindano ya kuwahi kupost humu?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.