Wazazi/walezi wengi hutamani kujenga tabia mbalimbali nzuri kwa watoto lakini hujikuta katika njiapanda ya kuchagua tabia ipi waiwekezee nguvu zaidi ya nyingine. Katika kuhudumia kwangu wazazi kwa kuwapa ushauri kwa miaka zaidi ya sita sasa nimekutana na wazazi wengi ambao wanajua tabia gani...
Sawa. Binafsi nimekutana nao, ni wengi. Sio mabubu, wanahitaji msaada tu. japo kwa umri huo unakuwa umechelewa sana. Jamii inadanganyana kwamba sio kitu kibaya mtoto kuchelewa. Wazazi wahimizwe kuwasaidia watoto mapema.
nakutana na watoto wenye miaka mpaka saba hawajaweza kuongea. Unadhani wataanza shule muda gani? kuchelewa kuongea kusipopewa suluhisho kunaweza kumfanya mtoto awe nyuma kwenye kila kitu. Pia, watoto wanaochelewa kuongea kwasababu ya autism usipowatafutia suluhu huwa hawawezi kutumia lugha...
1. Kujiongelesha mwenyewe. Jiongeleshe mtoto akiwa karibu juu ya mambo unayoyafanya. Mfano, naosha vyombo sasa, napika chakula, nafagia nyumba.
2. Simama, mpe mtoto muda wa kujibu. Unapozungumza na mtoto, kaa kimya, mpe nafasi ya kujibu. Akishindwa kujibu msaidie kujibu kisha mtake arudie...
Swali kubwa ninaulizwa na wazazi/walezi kila siku juu ya matatizo ya watoto kuchelewa kuongea ni: Nani anaweza kunisaidia kulimaliza tatizo hili la kuchelewa kuongea kwa mtoto wangu?
Binafsi huwa nakosa jibu rahisi la kuwapa wazazi/walezi moja kwa moja mpaka nimuone mtoto na shida yake ni ipi...
Mpeleke kwenye hospital yoyote yenye audiologist mzuri amkague kwanza. Majibu atakayokupa unaweza kushare na mimi kupitia 0765886191. Lakini pia, unaweza kunitumia video clip ambayo mtoto anaongea, anaongeleshwa na kuagizwa kitu au kupewa maelekezo fulani. Ni ngumu kwa mimi kukwambia chochote...
Naandika mara kwa mara hapa. Nitaandika juu ya suluhisho muda ujao. Ninaenda kuedit hitimisho ili watu wajue kuwa nitaandika wakati ujao. Japo napendekeza utumie lugha nzuri, hakukuwa na haja ya kejeri. Tumia lugha nzuri muda ujao kama ipo kwenye sehemu ya maadili yako.
Sijapaniki, ni ngumu kupaniki kwa jambo dogo kiasi hicho. Nimeonesha msisitizo tu. Umeonesha mzaa kwenye jambo ambalo hauna uelewa nalo. Kuna wengine huwa hadi mabubu kwa kuchelewa kuongea tu, bila ya kutafutiwa tiba mapema.
TV inarudisha sana maendeleo ya ukuaji wa ubongo wa watoto. Nimefanya diagnosis kwa watoto wengi wenye tatizo hili, chanzo kwa wengi nimebaini ni TV. Nitaandika makala juu ya hili nikipata wasaa.
Umeisoma makala yote? Mtoto anayechelewa kuongea huwa katika hatari ya kuwa nyuma katika kila kitu. Nimesaidia watoto wa namna hiyo, kama haujawahi kusaidia wala kuwa na mtoto wa namna hiyo unaweza usione uzito wa tatizo. Usipende kurukia hitimisho rahisi kwenye matatizo sensitive kama haya...
Tatizo la watoto kuchelewa kuongea ni la miaka mingi sana lakini miaka ya hivi karibuni limeonekana kuongezeka kwa kasi sana siku hadi siku.
Kuchelewa kuongea ni moja kati ya matatizo ya mawasiliano ambayo huwakuta watoto: tatizo hili hujitokeza pale ambapo watoto hushindwa kuongea kuendana na...
Nimekuwa nikupokea maswali ya wazazi/walezi wengi hususani wanapoanza safari ya hii ya kuwajengea watoto wao tabia ya kupenda kujisomea vitabu lakini swali kubwa huwa ni: Je, mtoto wangu anaelewa ninachomsomea? Au mbona mtoto wangu aelewi ninachomsomea? Na mengine mengi yenye ufanano na hayo...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.