Nimeingizwa kwenye kundi linaitwa AFRIC INVESTMENT, wanataka niinguze hela na kuvuna kwa utaratibu kama ule wa DECI.
Anayelifahamu kundi hili atujuze, naona dalili ya kupigwa!!
Jamani, natambua umuhimu wa askari wetu katika kuongoza magari. Lakini napata shida kujua vigezo wanavyotumia kuweka upande mmoja zaidi ya nusu saa hadi saa nzima, bila kujali kuwa, kuna wanaowahi uwanja wa ndege au ni jioni ambapo magari mengi yanatoka mjini lakini ndiyo yanasubirishwa kwa muda...
Naona kuna kukatika umeme hasa ikifika jioni. Je, ni mgao pasipo kutaarifiana? Sasa hivi Tabata hakuna umeme na jana vile vile katika muda ule ule. Tiambiane ukweli.
Jamani, ni vema niwape tahadhari nyie vidume mnaotembelea Dom. Mji mkuu umevamiwa na machangu hataree wanaoweka dozi ya usingizi ya kulala hata siku tano hujitambui.
Wameshaua kadhaa na wala hawana uchungu wowote na madhara wanayoleta. Usihadaike na urembo, ni mbaya kuliko jambazi mwenye bunduki!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.